Na Mwandishi Wetu, Morogoro
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM )umesema
Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye hafahamu wala hajui mantiki na
dhana ya demokrasia ya vyama vingi ndiyo maana amekua akitoa madai ya
kitoto na shutuma za kuwepo ukandamizaji wa demokrasia nchini .
Kadhalia Umoja huo umeeleza kuwa kwakuwa Sumaye hajui na
wala haelewi mipaka na mizania itokanayo na demokrasia, amejikuta
akiishutumu bila ushahidi serikali ya Rais Dk John Magufuli akiongozwa
na msongo wa chuki, hamaki na choyo.
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu
Shaka ameyasema hayo jana aliposimama kusalimiana na Vijana wa CCM
Mvomero Morogoro wakati akielekea Dodoma kufuatia madai ya Sumaye akidai
watawala hawataki katiba mpya na nchi ina mfano wa mgumu wa vyama vingi
vya siasa.
Shaka alisema mantiki au msingi wa kuruhusiwa vyama vingi
nchini si kukwamisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii au kuwafanya
wananchi kila siku wakusanyike viwanjani kusikiliza mikutano ya hadhara
bila kutilia maanani uzalishaji mali viwandani, mashambani na
maofisini.
Alisema aina yoyote ya demokrasia ambayo itakakosa ukomo ,
adabu, mipaka. mizania na ustaarabu, huweza kujibadili na kupoteza
uhalisia wake au heshima katika jamii ikiwemo kuwafanya watu wasijue
uyakini wa dhana yenyewe.
" Vijana wenzangu hata ligi ya soka au mashindano ya
kutafuta warembo yana msimu na vipindi vyake, timu haziwezi kushiriki
michuamo mwaka mzima bila wachezaji na waamuzi kupumzika, domokrasia ya
wapi ambayo haina vipindi vya kampeni, uchaguzi au watu kutakiwa kufanya
kazi za maendeleo acheni kusikiliza poroja za wanasiasa waliochoka
vijana chapeni kazi sasa ili kujiletea maendeleo endelevu" Aliwasa Shaka
.
Alisema UVCCM imeshangazwa na matamshi ya Sumaye anayedai
kuwa serikali ya awamu ya tano inakandamiza misingi ya demokrasia
kwasababu tu imevitaka vyama kuendesha shughuli za kisiasa kwenye
mikutano ya ndani ili kuwapa nafasi wananchi kujituma na kuzalisha.
Kaimu huyo Katibu Mkuu alisema hata kanuni na fomula za
masomo ya hesabu, kemia na baiolojia hazilingani katika kupata majawabu
halisia hivyo akataka ifahamike demokrasia nayo ina vipindi vya kampeni
, mikutano ya hadhara, uandikishaji, upiga kura,kuhesabu na kutangazwa
matokeo .
"UVCCM tunamfahamu Sumaye toka akiwa Naibu Waziri wa Kilimo
hadi Waziri Mkuu, hana rekodi nzuri ya kiutendaji ilioleta tija,
mafanikio au ufanisi katika maeneo aliyoyaongoza, yaonyesha ni mshabiki
wa hadithi kuliko kufanya kazi "Alisistiza.
Aidha alimtaka mwanasiasa huyo kufuta ndoto na fikra siku
moja itatokea CCM kudondoka madarakani kisha yeye au mshirika wake
Edward Lowassa mmoja kati yao awe urais au mgombea yeyote kupitia
Chadema na Ukawa .
"Tanzania imechoka kuwa ombaomba wa kila msaada toka kwa
wahisani na washirika wa maendeleo, Serikali ya CCM imezinduma
usingizini na kujitambua, haitaruhusu upuuzi usio na manufaa ili
ionekane demokrasoa maana yake ni mikutano ya hadhara bila
uzalishajimali nakutakeni vijana popote mlipo nchini kila mmoja afanye
kazi tumuunge mkono kwa vitendo Rais wetu Dk John Pombe Magufuli
anawapenda sana vijana na anatamani kuona mnafanikiwa katika ndoto zenu
za kuinua kipato kwa kujituma na kufanya kazi kwa bidii "Alisisistiza
Shaka.
Kaimu huyo Katibu Mkuu alieleza kuwa Waziri Mkuu huyo
Mstaafu anatatapata na kutoa matamshi yenye ukakasi unaoambatana na
fitna kwa matarajio ya kuzifarakanisha jumuiya za kimataifa na Serikali
za CCM ili zionekane haziheshimu demokrasia wakati si dai la kweli.
"Sumaye na Chadema wakati wakitoa matamshi hayo ya kitoto
na kudai demokrasia haipo bila katiba mpya, nchi wahisani, taasisi za
nje, mashirika ya kimataifa na washirika wa maendeleo, wanapongeza
utendaji wa Rais na Serikali yake" Alieleza
Hata hivyo Shaka alimtaka Sumaye kuachana na siasa za
kizamani kwasababu hata ushiriki wake akiwa Chadema haumjengei heshima
na uaminifu kutokana na udhaifu wa kumbukumbu zake toka akiwa kiongozi
wa juu wa Serikali kabla ya kuhamia upinzani na kusaka madaraka huku
akiwa hakubaliki.
Sumaye mwishoni mwa wiki alitoa matamshi yanaiponda
serikali ya ccm wakati akizungumza katika mahafali ya vijana wanafunzi
wafuasi wa chadema (CHASO) jijini Dar es Salaam huku akiinanga Serikali
ya Rais Dk Magufuli kwa madai ya kukwepa kuhusisha mchakato wa katiba
inayopendekezwa na madai ya kukandamiza demokrasia ya vyama vingi kwa
kuzuia mikutano ya hadhara na maandamano ya amani.
End
Source Zanzibar Leo
0 Maoni