Unordered List


KATIBU MKUU WA CCM ABDULRAHMAN KINANA AKAGUA MIRADI MBALIMBALI NA KUZUNGUMZA NA WANANCHI KISHAPU

1Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na Suleiman Nchambis Mbunge wa Jimbo la Kishapu katika mji wa Maganzo wakati alipowasili rasmi katika Wilaya ya Kishapu leo na kutembelea kata kadhaa akiongozana na Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi Ndugu Nape Nnauye Kushoto pamoja na uongozi wa mkoa wa Shinyanga hayupo pichani katika kuimarisha chama utekekelezaji wa Ilami ya Uchaguzi ikiwa ni pamoja na kuhimiza wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo wilayani humo.PICHA NA KIKOSI KAZI CHA FULLSHANGWE-KISHAPU 3Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman akisalimiana na wananchi wakati alipowasili katika jimbo la Kishapu mji wa Maganzo leo asubuhi, Kulia ni Suleiman Nchambis Mbunge wa jimbo la Kishapu na katikati ni Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi Ndugu Nape Nnauye 5 Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi Ndugu Nape Nnauye akiwa amepakizwa kwenye baiskeli mara baada ya msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kupokelewa na wananchi wa kata ya Mwigumbi ambako alitembelea miradi ya maji na ujenzi wa nyimba ya mwalimu na maabara katika shule ya sekondari Mwigumbi. 6Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Mbunge wa jimbo la Kishapu Ndugu Suleiman Nchambis wakishiriki kuchekecha mchanga huku Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi akiweka mchanga katika chekecheo wakati walipotembelea na kukagua ujenzi wa nyumba ya mwalimu na jengo la Maabara katika shule ya Sekondari Mwigumbi. 7Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kulia na Mbunge wa jimbo la Kishapu Ndugu Suleiman Nchambis wakiendelea kuchekecha mchanga kwa ajili ya ujenzi wa maabara ya shule hiyo. 9Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipaka rangi katika kuta za jengo la maabara ya shule hiyo ikiwani kuhamasisha wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo ili kuleta tija katika utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa nchini. 11Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana naMwenyekiti wa CCM Mkoani Shinyanga Ndugu Khamis Mngeja wakishiriki kucheza ngoma za nyoka mara baada ya kupokelewa katika eneo la mradi wa maji safi uliojengwa katika kijiji cha Mwigumbi Kata ya Mondo 12 Mbunge wa jimbo la Kishapu Ndugu Suleiman Nchambis akishiriki kucheza ngoma ya kucheza na nyoka katika kijiji cha Mwigumbi. 13Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Mbunge wa jimbo la Kishapu Ndugu Suleiman Nchambis wa tatu kutoka kulia na Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye wa pili kutoka kushoto kuelekea mahali ambapo mradi wa maji umezinduliwa katika kijiji cha Mwigumbi. 14Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kuzindua rasmi mabomba ya maji katika kijiji cha Mwigumbi kulia ni Mbunge wa jimbo la Kishapu Ndugu Suleiman Nchambis na kushoto Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye. 15Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akifungua koki ya bomba kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji katika kijiji hicho kushoto ni Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye na kulia ni Mbunge wa jimbo la Kishapu Ndugu Suleiman Nchambis wakishuhudia tukio hilo. 16Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimtwisha ndoo ya maji Bi Rebeca Sayayi mara baada ya kuzindua rasmi uchotaji wa maji katika mabomba hayo. 17Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye akimtwisha ndoo ya maji Bi.Eda Nyangiru ndoo ya maji mara baada ya kuzinduliwa kwa mabomba hayo. 18Vijana wakinywa maji ya kunywa kwa kushirikiana chombo kimoja 19Jengo la Maabara katika shule ya sekondari Mwigumbi Wilayani Kishapu. 20Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa Mwingumbi 21Mbunge wa jimbo la Kishapu Ndugu Suleiman Nchambis akiwahutubia wananchi wa Mwigumbi. 22Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na ujumbe wake wakipokelewa na kikundi cha ngoma za asili mara baada ya kuwasili katika eneo la mkutnano mjini Kishapu leo ambapo mkutano wa hadhara umefanyika. 23Mbunge wa jimbo la Kishapu Ndugu Suleiman Nchambis akishiriki kucheza ngoma huku Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishuhudia tukio hilo.

24Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye akishiriki kupiga ngoma wakati kikundi cha ngoma za asili kikitumbuiza katika mkutano huo. 25Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye akiwahutubia wananchi wa mjini Kishapu. 26Balozi wa China nchini Tanzania Lu younging akisalimia wananchi katika mkutano huo wa hadhara huku Nape Nnauye akitafsiri kwa wananchi katikati ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana. 27Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika mji wa Kishapu 28Mbunge wa jimbo la Kishapu Ndugu Suleiman Nchambis ,Balozi wa China nchini Tanzania Lu younging,Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Khamis Mngeja wakishiriki kucheza ngoma za asili katika mkutano huo. 30,Balozi wa China nchini Tanzania Lu younging na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana huku Mbunge wa Jimbo la Kishapu Suleiman Nchambis akicheza kulia anayeshuhudia ni Nape Nnauye na kushoto ni mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Khamis Ngeja 31Balozi wa China nchini Tanzania Lu younging,Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakizungumza jambo wakati walipokagua ujenzi wa majengo ya hospitali ya Wilaya ya Kishapu mjini Kishapu leo, kushoto ni Mbunge wa jimbo la Kishapu Ndugu Suleiman Nchambis. 32Hili ni moja ya majengo ya hospitali hiyo ambayo yako katika hatua za mwisho za ujenzi.

Chapisha Maoni

0 Maoni