Unordered List


SIXTUS MAPUNDA NDIYE KATIBU MKUU UVCCM

Katibu Mkuu aliyemaliza muda wake Martin Shigela akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Ndugu Mboni Muhita kabla ya kuanza kwa kikao cha wajumbe wa baraza la Umoja wa Vijana katika Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.


Mtela Mwampamba akiwasili kwenye uwanja wa CCM Afisi Kuu za CCM Zanzibar tayari kuhudhuria kikao cha Baraza Kuu la Vijana Taifa.

Mjumbe wa Baraza la Vijana Taifa  Antony Mavunde akisaliminiana na Mjumbe wa Baraza kutoka Jumuiya ya Wazazi William Malecela nje ya jengo la Afisi Kuu ya CCM Zanzibar kabla ya kuanza kwa kikao cha Baraza la Vijana Taifa.
Wajumbe wa Baraza la Vijana wakicheza ngoma ya Boso yenye asili ya Kusini Pemba, kabla ya kuanza kikao cha Baraza Kuu la Vijana.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Balozi Seif Idd akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katika viwanja vya Afisi Kuu ya CCM Zanzibar ambapo Makamu wa Pili wa Rais ndiye aliyekuwa Mgeni rasmi.
Viongozi Wakuu wa CCM wakiomba Dua mbele ya kaburi la Muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar Sheikh Abeid Aman Karume kabla ya kuanza kwa kikao cha Baraza la Vijana la CCM Taifa.


January Makamba akizungumza na Wajumbe wa Baraza laVijana wa CCM kabla ya kuanza kwa kikao cha Baraza.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Dk.Emmanuel Nchimbi akitoa salaam kwa wajumbe wa Baraza kuu la Vijana Taifa kabla kuanza kwa kikao cha Baraza Kuu la Vijana wa CCM
Mjumbe wa Kamati Kuu Mohamed Seif Khatibu akiwasalimu wajumbe wa Kikao Cha Baraza Kuu la Vijana la Taifa kwenye ukumbi wa mikutano CCM Zanzibar.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Sadifa Juma Hamisi akisoma risala kabla ya kumkaribisha Balozi Seif Idd kufungua kikao cha Baraza la Umoja wa Vijana.


Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Idd akitoa hotuba ya kufungua kikao cha Baraza Kuu la CCM Vijana leo 1/9/2013 katika ukumbi wa mkutano wa Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.



Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Ndugu Sixtus Mapunda akizungumza kwa mara ya kwanza na wajumbe wa Baraza la Vijana wa CCM .

 Meza Kuu ikiwa na Katibu Mkuu mpya aliyechaguliwa Sixtus Mapunda wakati wa kikao cha Baraza la Vijana kilichofanyika Zanzibar.
Wajumbe wa Mkutano wa Baraza kuu la CCM wakiserebuka baada ya kuidhinisha kuwa Sixtus Mapunda ndiye Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo ya CCM.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimkubatia Katibu Mkuu wa umoja wa vijana aliyemaliza muda wake Ndugu Martin Shigela,kulia niKatibu Mkuu mpya wa UVCCM akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar) Vuai Ali Vuai .

Chapisha Maoni

0 Maoni