Unordered List


Zitto-Kabwe_bec88.jpg
*Apanga kuanika aliyobaini Ulaya, ashtushwa na fedha zilizofichwa visiwa vya Uingereza
*Asema ni zaidi ya zile za Uswisi, ayageukia makampuni asema nayo yamo, aonya yakiachwa
MIEZI 12 tangu serikali iazimie kuunda timu maalumu kuchunguza sakata la vigogo wanaodaiwa kuficha fedha haramu nje ya nchi, hususani katika mabenki ya Uswisi, upepo wa suala hilo sasa unaweza kubadilika wakati wowote, baada ya muasisi wa hoja hiyo, Zitto Kabwe, kupanga kuibua mazito aliyodai kubaini katika uchunguzi wake Ulaya.
Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini (Chadema), alirejea nchini jana akitokea katika nchi za Ulaya, baada ya kumaliza kazi ya kuongoza jopo la wataalamu kutoka Shirika la Kimataifa la Mtandao wa Ulaya wa Madeni na Maendeleo (Eurodad), kufanya uchunguzi kuhusu masuala ya uwazi katika kodi.(P.T)

Chapisha Maoni

0 Maoni