Unordered List


MKE WA RAIS, MAMA SALMA KIKWETE AHUDHURIA MKUTANO WA WANAWAKE AFRIKA MASHARIKI NA KATI NA ASIA

MKE WA RAIS, MAMA SALMA KIKWETE AHUDHURIA MKUTANO WA WANAWAKE AFRIKA MASHARIKI NA KATI NA ASIA

 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokewa na Mwanzilishi na Afisa Mtendaji Mkuu wa CEO Clubs Network, Bwana Tareq Ahmed Nizami,
mwandaaji mwenza wa Mkutano wa  Wanawake kutoka Afrika, Mashariki ya Kati na Asia, 'The Africa -Middle East-Asia' unaofanyika katika Hoteli ya Atlantis The Palm, huko Dubai katika Jamhuri ya Falme za Kiarabu (UAE), tarehe 16.12.2013. Mwandaaji mwingine wa mkutano huo ni Kituo cha Maendeleo ya Kiuchumi na Uongozi (CELD).
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mama Penehupifo Pohamba, Mke wa Rais wa Namibia wakati wa ufunguzi wa mkutano wa siku tatu wa  wanawake kutoka Afrika, Mashariki ya Kati na Asia unaofanyika Dubai kuanzia tarehe 16.12.2013.
  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizungumza na Balozi wa Tanzania katika nchi za Falme ya Kiarabu (UAE) wakati wa sherehe za ufunguzi wa Mkutano wa wanawake kutoka Afrika, Mashariki ya Kati na Asia unaofanyika katika hoteli ya Atlantis The Palm iliyopo Dubai, Jamhuri ya Falme za Kiarabu tarehe 16.12.2013. Kushoto kwa Mama Salma ni Mke wa Rais wa Namibia Mama Penehupifo Pohamba, na wa kwanza ni Mshauri Maalum wa Mama Pohamba Mchungaji Justina Hilukiluah na wa mwanzo kushoto no Bwana Tariq Nizami, Mwanzilishi na Afisa Mtendaji Mkuu wa CEO Clubs Network.



 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwasilisha mada ya Elimu: Key to the Future of Women in Emerging Economies, kwenye mkutano wa siku tatu wa Wanawake kutoka Afrika, Mashariki ya Kati na Asia unaofanyika huko Dubai tarehe 16.12.2013.
 Mke wa Rais wa Namibia Mama Penehupifo Pohamba akimpongeza Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete baada ya kutoa mada iliyosisimua wajumbe wa Mkutano wa Wanawake kutoka Afrika, Mashariki ya Kati na Asia unafanyika jijini Dubai, Jamhuri ya Falme aza Kiarabu tarehe 16.12.2013.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa na Mheshimiwa Margaret Zziwa, Spika wa Bunge la Afrika Mashariki. Viongozi hao ni miongoni mwa viongozi wanawake kutoka Afrika, Mashariki ya Kati na Asia wanaohudhuria mkutano wa siku tatu huko Dubai.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akifanya mazungumzo na Dr. Angela Moore, Balozi wa Heshima kutoka Jimbo la Georgia, nchini Marekani wakati wa mkutano wa wanawake kutoka Afrika, Mashariki ya Kati na Asia huko Dubai tarehe. PICHA NA JOHN LUKUWI

Chapisha Maoni

0 Maoni