"Wananchi wa Nzega zaidi ya 1000 wamesaini azimio letu la mkutano wa hadhara uliofanyika juzi kupinga azimio juu ya azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani kutaka kuzigawanya pesa za Resolute kwenye kila kata, ambapo tayari baadhi ya madiwani wasio waadilifu wamejipanga kuzila pesa hizi kutokana na historia ya matumizi ya pesa za mfuko wa jimbo ambapo wengine hawakutekeleza miradi iliyokusudiwa na walizila tu! alisema HK.
Moja kati ya Mabango hayo linasema " TUNAUNGA MKONO MAWAZO YA MBUNGE,
FEDHA HIZO KUNUNUA VIFAA KWA AJILI YA MAENDELEO YA WANANZEGA" hakika
wananchi wa Nzega wamechaluka duuuu
Unaweza Kuona Wananchi wa Nzega waliwa ktk MaandamanoKutoka Mjini,
Katikati ya Mji na kuelekea Mahakama ilipo Bomani wilayani Nzega, Wakiwa
wamebeba Mabango yenye Jumbe tofauti tofauti Kupinga Madiwani kutaka
kugawana pesa hizo na kumuunga Mkono mbunge! Pesa hizo zitumike Kununua
Vifaa vya Ujenzi wa Barabara na vifaa vingine vya maendeleo ya
Nzega....!!
Hapa ni katika Moja ya Vikao hivo vya Hadhara vya Mbunge na Mwenyekiti
wa TAMISEMI alivyofanya Nzega, ktk Moja ya taratibu za Kuelimisha
wananzega kuhusiana na Pesa hizo
Mbunge
Kigwangalla akiwa Kabebwa Juu juu na Wana Nzega Baada ya Maandamano ya
juzi baada ya mkutano wa hadhara viwanja vya parking Nzega
kupinga maamuzi ya kuzigawana pesa za ushuru wa huduma TZS 2.452 bn,
Wananchi waliandamana na Mbunge Dk, Hamisi Kigwangala Mpaka Bomani ilipo
Mahakama!
"Kwa kuwa nilianza Ubunge na Mungu, nina hakika nitamaliza naye. Mahakama
imetupa ushindi kwenye kesi ya kwanza iliyosikilizwa exparte"! Alisema Kigwangalla nilipokuwa nikizungumza nae hapo Jana!
Habari hii ilitoka ktk Gazeti la UHURU la Jana pia
0 Maoni