Unordered List


MAKAMU MWENYEKITI CCM (BARA) NA KATIBU MKUU WAWASILI MBEYA TAYARI KWA SHEREHE ZA MIAKA 37 YA KUZALIWA KWA CCM


 Makamu Mwenyekiti CCM(Bara) Ndugu Phillip Mangula akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya Ndugu Godfrey Zambi wakati wa mapokezi kwenye ofisi za CCM Mkoa,Makamu Mwenyekiti amewasili mkoani Mbeya tayari kwa maadhimisho ya sherehe za miaka 37 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi .
 Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Phillip Mangula akisalimiana na Kanali Mstaafu Limbo Masanja mara baada ya kuwasili kwenye ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya.
 Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Ndugu Phillip Mangula akijibu baadhi ya maswali ya waandishi wa habari baada ya kuwasili kwenye ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya tayari kwa sherehe za miaka 37 ya kuzaliwa kwa CCM zitakazofanyika tarehe 2 Februari kwenye uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoka nje ya uwanja wa ndege wa Songwe mkoani Mbeya akiongozana na Mwenyekiti wa wilaya ya Momba Ndugu Juma Yusufu Rashid na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya Godfrey Zambi.
 Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mbeya Dk. Mary Mwanjelwa akibadilishana mawazo na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Dogo Idd Mabrouk nje ya ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye akizungumzwa na baadhi ya waandishi wa habari waliofika mkoani Mbeya kwa ajili ya kuapata habari na matukio mbali mbali yatakayojiri wakati wa sherehe za miaka 37 ya CCM.
Bidhaa za CCM zikiwa kwenye soko sambamba na maandalizi ya sherehe za miaka 37 ya kuzzaliwa kwa CCM zinazofanyika kitaifa mkoani Mbeya.

Chapisha Maoni

0 Maoni