Unordered List


VIKUNDI VYA VICOBA VILIYOPO CHINI YA POVERTY FIGHTING TANZANIA(PFT) INAYOSIMAMIWA NA MBUNGE WA TEMEKE ABBAS MTEMVU VYAKABODHIWA VIFAA VYA MILLIONI 192.3


*NI GARI SITA AINA YA SUZUKI CARRY,  *BAJAJ KUMI, *PIKIPIKI 19 AINA YA BOXER, *PIKIPIKI YA MZIGO AINA YA TOYO, *VIFAA VYA UMEME VYA USEREMALA, *MBAO, *VIFAA VYA STATIORIES NA VIFAA VYA SHOOTING CAMERA
Vifaa vikiwa tayari kukabidhiwa kwa vikundi hivyo vya Vicoba chini ya PFT
 Baadhi ya sare zilizovaliwa na wadau zilikuwa na ujumbe huu
  Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwezeshaji na Uwekezaji. Dk. Mary Nagu (kushoto) akiwasili ukumbini huku akiwa na Mwenyekiti wa PFT, Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu, kwa ajili ya kuvigawia vifaa mbalimbali  vikundi 130 vya Vikoba vilivyo chini ya Taasisi ya PFT katika hafla iliyofanyika leo kwenye Ukumbi wa PTA, Sabasaba, Dar es Salaam
 Mwenyekiti wa PFT, Mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu akimtambulisha kwa waziri Nangu, Mwezeshaji wa VICOBA walioko chini ya PFTJohannes Linde wakati waziri Nagu alipowasili ukumbini.
 Wanavikundi wakilipuka kwa shamrashamra wakati wa mapokezi ya waziri Nagu ukumbini
 Cherekochereko na mabango
 Kina mama wa Vicoba wakifurahi
 Mama Mtemvu na Mwanae wakiwa kwenye hafla hiyo
 Wanachama wa Vicoba wakiwa wamekaa baada ya mapokezi
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Juma Kassim 'Juma Nature' akitumbuiza wakati wa hafla hiyo.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Juma Kassim 'Juma Nature' akitumbuiza kwenye hafla hiyo
 Msanii Snura Mushi maarufu kwa jila na Majanga, akikonga nyoyo za wanavicoba wakati wa hafla hiyo
 Snura Majanga akionyesha umahiri wake mbele ya wana-Vicoba
 Mwenyekiti wa PFT, Mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu akimkabidhi Waziri Nagu hati maalum ya shukrani kwenda kwa Rais Jakaya Kikwete kutokana na mchango alioutoa wa sh. milioni 50 kwa PFT. Kushoto ni Naibu Waziri wa Maendeleo na Jamii Jinsia na Watoto Pindi Chana.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwezeshaji na Uwekezaji). Dk. Mary Nagu (katikati) akikabidhi pikipiki kwa moja ya vikundi 130 vya Vikoba vilivyo chini ya Taasisi ya PFT katika hafla ya kuviongezea uwezo kwenye Ukumbi wa PTA, Sabasaba, Dar es Salaam leo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Temeke, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi hiyo, Abbas Mtemvu.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwezeshaji na Uwekezaji). Dk. Mary Nagu (katikati) akikabidhi gari kwa moja wa viongozi wa PFT.
Masiriamali ambaye ni mwanachama wa moja ya vikundi cya Vicoba vilivyopo chini ya PFT akiwa kazini wakati wa hafla hiyo
 Wanachama wa Vicoba wakichangamkia fomu za NSSF za Matibabu
 Wanakikundi cha Vicoba wakiwa kwenye gari lao baada ya kukabidhiwa
 Mweneyekiti wa PFT, Mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu akizungumza na waandishi wakati wa hafla hiyo
Mtembu akiwa na Kina Juma Nature na Snura Majanga ambao walitumbuiza kwenye hafla hiyo. KUPATA MAELEZO KAMILI KUHUSU HAFLA HIYO NA PFT>

 

Chapisha Maoni

1 Maoni

Unknown alisema…
pongezi kwa mhe.mtemvu mbunge wa temeke kwa juhudi na ubunifu unawawezesha vijana kiuchumi:

[ Wakati wengine wanawatumia vijana kwa mambo hasi kama fujo na vurugu na kuwakatisha tamaa,CCM inawawezesha kwa mambo chanya huku ikiwahamasisha kutumia akili na maarifa kupambana na changamoto zinazowakabili]