Unordered List


MWENYEKITI WA CCM TAIFA AWASILI MKOANI MBEYA TAYARI KWA SHEREHE ZA MIAKA 37 YA KUZALIWA KWA CHAMA CHA MAPINDUZI


 Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano akipunga mkono wakati akishuka kutoka kwenye ndege jioni ya leo kwenye uwanja wa Kimataifa wa Songwe mkoani Mbeya tayari kwa sherehe za kuzaliwa kwa CCM zitakazofanyika tarehe 2 Februari ambapo asubuhi kutakuwa na matembezi ya mshikamano kisha kuhitimishwa kwenye uwanja wa wa Sokoine.
 Mwenyekiti wa CCM Taifa,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Ndugu Phillip Mangula mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe tayari kwa maadhimisho ya sherehe za miaka 37ya kuzaliwa Chama Cha Mapinduzi.
 Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Ndugu Abdallaha Bulembo mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa kimataifa wa Songwe mkoani Mbeya tayari kwa sherehe za kutimiza miaka 37 tangia kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi.
Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mbeya Mjini Ndugu Ephraim Mwaitenda kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe mkoani Mbeya.
 Boda Boda zikiongoza msafara wa Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete aliyewasili mkoani Mbeya kwa ajili ya sherehe za miaka 37 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi.

 Bodaboda zikiongoza msafara wa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete kutoka kwenye uwanja wa kimataifa wa Songwe.

Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete(katikati) akiwa kwenye ukumbi wa mikutano wa CCM mkoa wa Mbeya tayari kuongoza kikao cha Halmashauri Kuu ya mkoa wa Mbeya.

Chapisha Maoni

0 Maoni