Unordered List


TASWIRA KATIBU MKUU WA CCM NA NAIBU KATIBU MKUU CCM BARA WAKATI WA KAMPENI ZA CCM KALENGA


Katibu Mkuu CCM Taifa (Kulia) Kanali Mstaafu Kinana na Naibu Katibu Mkuu CCM-Bara (Kushoto) Mh.Mwigulu Nchemba Wakimnadi Mgombea wa CCM Jimbo la Kalenga Ndugu Godfrey William Mgimwa(Katikati) hii leo Kwenye Mkutano wa Hadhara wa Kampeni za Uchaguzi Uliofanyika Kata ya Magulilwa,Kijiji cha Magulilwa.Mapokezi ya Msafara wa Mgombea wa Jimbo la Kalenga-CCM akibebwa Juu Juu akiingia kwenye Uwanja wa Mkutano wa Kampeni hapa Magulilwa.Mh.Deo Filikunjombe akizungumza na Wananchi wa Kata ya Magulilwa hii leo wakati wa kampeni za Kumnadi Godfrey William Mgimwa.Mh.Deo amesisitiza Wanakalenga kuachana na Kelele za Wapinzani Kwasababu wamejaa maneno na Sio Vitendo.Yeye kama Mbunge wa Mkoa wa Iringa wanatambua Mchango Mkubwa auliofanywa na Marehemu Mgimwa kwenye Jimbo la Kalenga.Hivyo hakuna haja ya Kufanya Mabadiriko ya kuwapa Wapinzania ilihali Jimbo la Kalenga Ilani yake imetekelezwa Vizuri sana na bado Godfrey Mgimwa atamalizia yale yaliobakia kwenye Utekelezaji wa Ilani.Mh.Kangi Lugola akizungumza na Wananchi wa Kata ya Magulilwa hapa Kalenga na Kusisitiza kuwa ametoka Mwibala kwaajili ya Kuhakikisha Wanakalenga hawatoi nafasi kwa Wapinzani kwasababu Bungeni wamekuwa ni Kero kwa Kukosa nidhamu na Heshima kwa Umma wa Watanzania.
Mh.Mgimwa ambaye ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii akizungumza na Wananchi wa Magulilwa hii leo wakati wa Mkutano Wa Kampeni hapa Kalenga.
 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Bi.Jesca akiomba kura kwa Wanamagulilwa hapa Kalenga kwaajili ya Godfrey William Mgimwa Tar.16/03/2014 siku ya Uchaguzi.
 Naibu katibu Mkuu CCM-Bara akizungumza na Wananchi wa Kata ya Magulilwa hii leo Kwenye Mkutano wa Kampeni Jimbo la Kalenga.
Sehemu ya Wananchi waliofika Kwenye Mkutano Wakionesha ishara ya Kwenda Kumpigia Kura Godfrey William Mgimwa Tar.16/03/2014.Mmoja Wa Wananchi akionesha gazeti alilokuwa anasoma lililobeba Ujumbe Kuhusu Siasa Chafu Zinazofanywa na Chadema Jimbo la Kalenga.Kusho na Kulia ni Wagombea Wenza kwenye Kura za Maoni CCM wakati wa Kuchagua Mwana-CCm atakaye Gombea Ubunge jimbo la Kalenga.Wagombea Wenza hawa wamekuwa Bega Kwa Bega na Godfrey William Mgimwa kwenye Kampeni hizi ikionesha wazi CCM ni Wamoja.Mgombea wa Ubunge Jimbo la Kalenga Godfrey William Mgimwa akiomba Kura kwa Wananchi wa Kata ya Magulilwa hii leo.
Naibu Katibu Mkuu CCM Bara akifurahia Jambo na Mbunge wa Mwibala Mh.Kangi Lugola hii leo wakati wakuahirishwa kwa Mkutano wa Kampeni Kata ya Magulilwa Jimbo la Kalenga.Hatimaye Mkutano Umemalizika hapa Kata ya Magulilwa,Katibu Mkuu akiwa anaondoka na timu yake hapa Magulilwa.

Chapisha Maoni

0 Maoni