Unordered List


MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AONGOZA WAOMBOLEZAJI MSIBA WA MAALIM MUHIDIN GURUMO, JIJINI DAR


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mwanamuziki mkongwe, Kassim Mapili, na baadhi ya waombolezaji wakati alipowasili nyumbani kwa marehemu Maalim Muhidin Gurumo, Mabibo jijini Dar es Salaam, kwa ajili kuaga mwili wa marehemu kabla ya kusafirishwa kuelekea Kijijini kwao Masaki Wilaya ya Kisarawe kwa maziko,  Aprili 15, 2014. Picha na OMR
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na wanafamilia wa marehemu Maalim Muhidin Gurumo, wakati alipofika nyumbani kwa marehemu, Mabibo jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kuaga mwili wa marehemu kabla ya kusafirishwa kuelekea kijijini kwao Masaki Wilaya ya Kisarawe kwa maziko,  AprilI 15, 2014. Kulia ni Mjane wa marehemu, Pili Binti Saidi Kitwana. Picha na OMR
 Sehemu ya waombolezaji wakiwa nyumbani kwa marehu wakati wa shughuli ya kuaga mwili wa marehemu. Picha na OMR
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na waombolezaji katika msiba wa Maalim Muhidin Gurumo, wakati alipofika nyumbani kwake Mabibo jijini Dar es Salaam,  Aprili 15, 2014 kwa ajili ya kuaga kabla ya kusafirishwa kuelekea kijijini kwao Masaki Wilaya ya Kisarawe kwa maziko. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na waombolezaji wakati akiondoka nyumbani kwa marehemu Maalim Muhidin Gurumo, baada ya kuaga mwili wa marehemu. Picha na OMR

Chapisha Maoni

0 Maoni