Unordered List


ZIKIWA ZIMEBAKI SIKU CHACHE KUFIKIA UCHAGUZI WAPINZANI WAZIDI KURUDI CCM CHALINZE


  • 11 warudi CCM kwenye mikutano ya kampeni za Ubunge,akiwemo Mwenyekiti wa CUF Kata ya Msata Ndugu Idd Njema. 
  • Ridhiwani awaambia wananchi wa Mkoko muda wa kutumia jembe la Mkono umekwisha ni wakati wa kuanza kutumia matrekta.
  •  Asisitiza juu ya mpango bora wa matumizi ya ardhi
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Kijiji cha Lugoba na kuwaambia Ridhiwani ni kijana anayehifahamu vizuri Chalinze na changamoto zake .
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimnadi Mgombea wa Ubunge Jimbo la Chalinze CCM Ndugu Ridhiwani Kikwete wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Lugoba.
 Mamia ya wakazi wa kijiji cha  Lugoba wakimsikiliza mgombea wa ubunge jimbo la Chalinze CCM  Ndugu Ridhiwani Kikwete wakati wa mkutano wa kampeni.
 Mbunge wa Shinyanga Mjini Ndugu Stephen Masele ambaye pia ni Naibu Waziri wa madini akihutubia wakazi wa kijiji cha Lugoba wakati wa kampeni za ubunge CCM jimbo la Chalinze.
 Mbunge wa Mchinga Ndugu Said Mtanda akihutubia wakazi wa Lugoba na kuwaambia Lugoba aliyosoma yeye miaka ya tisini ina tofauti kubwa na hii ya 2014 na kuwasihi wananchi wa Chalinze kushirikiana na Mbunge wa CCM katika kuleta maendeleo ya Jimbo hilo.
 Mgombea wa Ubunge wa jimbo la Chalinze Ndugu Ridhiwani Kikwete akikaribishwa kwa furaha kuhutubia wananchi wa kitongoji cha Madesa wakati wa mkutano wa kampeni za ubunge.
 Mr.

 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze Ndugu Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Wazee wa kijiji cha Mkoko wakati wa mkutano wa kampeni za ubunge.
 Ridhiwani akionyesha moja ya kadi za kutoka upinzani waliorudi CCM kutoka kitongoji cha Mabungo.
 Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze CCM Ndugu Ridhiwani Kikwete akipokea kadi kutoka kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF Kata ya Msata Ndugu Idd Njema ambaye amejiunga na CCM katikati ni Katibu wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro Ndugu Steven Kazidi ambaye pia ni meneja wa kampeni za Mgombea wa Ubunge Jimbo la Chalinze CCM.
Hadhara Charles maarufu kwa jina la Ronaldo akionyesha uwezo wake wa kucheza na mpira wakati wa mkutano wa kampeni za ubunge CCM jimbo la Chalinze uliofanyika katika kijiji cha  Pongwe Msungura.

Chapisha Maoni

0 Maoni