Unordered List


KINANA AANZA ZIARA MKOA WA MANYARA, AKUTANA NA SUMAYE NA MARY NAGU


                                                                                                                                                                       Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye akimlaki Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, katika mapokezi yaliyofanyika katika kijiji cha Gehandu, wakati Kinana alipowasili katika Wilaya ya Hanang, akitokea mkoani Singida, kwenda kuanza ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na kusikiliza kero za wananchi na njia ya kuzitatua katika mkoa wa Manyara, leo Mei 27, 2014. 
                                                                                                                                                                       Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akisalimiana na Mkuu wa wilaya ya Hanang Christina Mndeme wakati wa mapokezi hayo.
 Sumaye akimlaki Katibu wa NEC, Itikadi na Uenzi Nape Nnauye, katika mapokezi ya Kinana yaliyofanyika katika kijiji cha Gehandu, Wilaya ya Hanang, Manyara. Kushoto Mkuu wa wilata hiyo Mndeme
                          Kinana akisalimiana na Mbunge wa Hanang, Dk. Mary Nagu wakati wa mapokezi hayo
               Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akisalimiana na Katibu Tawala wa mkoa wa Manyara, Omar Chambo wakati wa mapokezi hayo.
               Nape akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Hanang
               Nape akisalimiana na Mbunge wa Babati Vijijini, Jeetuson Patel wakati wa mapokezi kuingia wilaya hiyo Hanang
 Mapokezi ya Kinana Kijiji cha Gehandu, Hanang Manyara
               Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akipokea saluti ya Vijana wa UVCCM, wakati wa mapokezi yake, Kijiji cha Gehandu, Hanang Manyara
               Kinana akiingia Hanang, Manyara 
               Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Christina Mndeme (kulia) akiwa na mabinti wa Kibarbaig wakati wa mapokezi ya Kinana. 
                   Vijana wa Kibarbaig wakionyesha ushupavu wao wa kuruka wakati wakimburudisha Kinana wakati wa mapokezi katika Kijiji cha Gehandu, wilayani Hanang
                  Binti wa Kibarbaig akiruka wakati yeye na wenzake wakitoa burudani kwenye mapokezi ya Kinana 
             Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akipiga misumari kwenye kenchi kwenye jengo la maabara ya shule ya Sekondari ya Mwahu Kata ya Kihandu, wilayani Hanang. Picha zote na Bashir Nkoromo wa CCM Blog

Chapisha Maoni

0 Maoni