Unordered List


KINANA AMALIZA ZIARA YAKE WILAYA YA UYUI

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kata ya Ufuluma wilaya ya Uyui  ambapo aliwaambia wananchi hao Kilimo cha Tumbaku kiondoe umasikini na si kuongeza umasikini kwa mkulima.

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kata ya Ufuluma wilayani Uyuni Mkoani Tabora .
 Mbunge wa Jimbo la Tabora Kaskazini Ndugu Shaffin Mamlo Sumar akihutubia wakazi wa kata ya Ufuluma kwenye mkutano wa CCM uliofanyika Ufuluma,wilayani Uyui mkoani Tabora.
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Fatma Mwassa akihutubia wakazi wa Ufuluma kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Ufuluma wilaya ya Tabora mkoani Tabora.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye baada ya kumaliza mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Ufuluma wilaya ya Uyui mkoani Tabora.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Uyui uliofanyika kata ya Ulolangulu.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Mhandisi wa Wilaya ya Uyui Eng.Stephen Nyanda kukagua  maabara ya shule ya sekondari ya Kata ya Ndono,wilaya ya Uyui mkoani Tabora. Katika mpango wa Serikali wa Matokeo Makubwa  Sasa wilaya ya Uyui imekamilisha maabara katika shule za kata tano na zingine sita kukamilishwa mwaka ujao wa fedha.

Chapisha Maoni

0 Maoni