Unordered List


KINANA APIGA KAZI JIMBONI KWA TUNDU LISSU, WANANCHI WALIA NA MBUNGE HUYO KUKWAMISHA MAENDELEO


Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia mkutano wa hadhara leo, Maei 21, 2014, kwenye Viwanja vya Stendi ya Ikungi, wilayani Ikungi mkoani Singida, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM, kusikiliza kero za wananchi huku akijadiliana nao njia za kuzitatua mkoani humo.
Katibu wa NEC, Itikadi na uenezi, Nape Nnauye akihutubia kwenye mkutano huo wa Ikungi
Wananchi wakishangilia kwenye mkutano huo wa CCM uliohutubiwa na Kinana kwenye Viwanja vya Stendi  Ikungi, Singida.
Mwananchi akiishangilia CCM baada ya kukabidhiwa kadi na Kinana kwenye mkutano huo
Aliyekuwa  Katibu wa tawi la Chadema, Ikungi, Ismail Gwau akitupa bendera ya chama hicho mbele ya Kinana na Nape baada ya yeye na wenzake kuamua kufunga tawi lote na kuhamia CCM wakati wa mkutano huo uliofanyika Stendi ya Ikungi.
Katibu huyo aliyekuwa wa Chadema akitupa pia kadi za chama hicho mbele ya Kinana wakati wa mkutano huo wa Ikungi
Gwau alionyesha kadi yake mpya ya CCM baada ya kupewa na Kinana kwenye mkutano huo
Kinana akihutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Makiungu, Ikungi, Mei 21, 2014
Nape akihutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Makiungu, Ikungi
Kinana akizungumza kwenye zahanati ya Kijiji, cha Kimbe, Ikungi baada ya kukagua ujenzi wa zahanati hiyo ambao umekamilika lakini zahanati imeshingwa kuanza kutoa huduma kutokana na  nyumba  ya mganga kutokamilika kujengwa kutokana na mbunge wa jimbo la Singida Mashariki Tundu Lisu na Diwani wake kudaiwa kuzuia wananchi kuchangia
Nape akiwa na mtoto Frank John (5) ambaye alimbeba alipomkuta wakati Kinana alipokagua zahanati hiyo,kwenye Kijiji cha Kimbe, Ikungi.
Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akishiriki kuvuna mazao kwenye shamba la Mjane Mayasa Mukhandi wa Kijiji cha Unyaghumpi Kata ya Mungaa, Ikungi, Kinana alipotembelea shamba hilo, leo, Mei 21, 2014.
Mjumbe wa Kamati Kuu, Khadija Aboud akishiriki kuvuna mazao kwenye shamba la Mjane huyo, Mayasa Mukhandi wa Kijiji cha Unyaghumpi Kata ya Mungaa, Ikungi
Nape akishiriki kuvuna mazao kwenye shamba la Mjane huyo, Mayasa Mukhandi wa Kijiji cha Unyaghumpi Kata ya Mungaa, Ikungi.
Kinana akimpatia Bi Mayasa Mukhando ambaye ni Mjane, fedha za kumsaidia kuvuna shamba lake,  katika Kijiji cha Unyaghumpi
Kinana akishiriki ujenzi wa shule ya msingi ya Unyahongi, Ikungi Singida akiwa katika ziara hiyo leo, Mei 21, 2014.
Wananchi wakijitolea kwenye shule ya msingi Unyahongi, Ikungi
Mkurugenzi wa kampuni ya Singida Agriculture Ltd, Ali Mohamed, (kushoto) akimpa maelezo Kinana katika shamba la kampuni hiyo la kilimo cha Umwagiliaji kwa matone, eneo la Mkiwa, Ikungi
Mkurugenzi wa kampuni ya Singida Agriculture Ltd, Ali Mohamed,akimpa maelezo Kinana eneo la Mkiwa, Ikungi
Msafara wa Kinana wakitazama bwawa la mradi wa kilimo cha umwagiliaji kwa matone kinachoendeshwa na kampuni ya Singida Agriculture Ltd, eneo la Mkiwa, Ikungi
Nape akijaribu kulima kwa trekta kwenye shamba la kampuni hiyo
Kinana akipatiwa maelezo na mkurugenzi wa kampuni hiyo ya Kilimo kuhusu wanavyohifadhi mazao kwenye makasha kabla ya kusafirisha.
Nape akisaidia kupanga kwenye vifaa maalum maharage yanayolimwa kwenye mashamba ya kampuni hiyo ya kilimo. Picha zote na Bashir Nkoromo, CCM Blog

Chapisha Maoni

0 Maoni