Unordered List


KINANA AWASILI PEMBA


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (ZNZ) Vuai Ali Vuai mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege Pemba, Katibu Mkuu anatarajiwa kufanya mkutano wa hadhara Pemba
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akisalimiana na Viongozi wa CCM Pemba mara baada ya kuwasili Pemba leo ambapo anatarajiwa kufanya mkutano wa hadhara utakaofanyika Gombani ya Kale.
 Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ukikatiza mitaa ya Madungu Flat.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisaini vitabu vya wageni kwenye afisi kuu ya CCM Pemba Chake Chake pamoja na Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wengine ofisini ni Naibu Katibu Mkuu CCM (ZNZ) Vuai Ali Vuai,Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kusini Ndugu Abdala Mshindo na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini Ndugu Mzee Mbelwa.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiangalia Buku la Wageni ( Kitabu cha Kusaini Wageni) cha Afisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Pemba
Buku la Wageni ( Kitabu cha Kusaini Wageni) cha Afisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Pemba.

Chapisha Maoni

0 Maoni