Unordered List


MH. MWIGULU NCHEMBA: NITAONGOZA MAPAMBANO YA KUMGOA MSIGWA


Naibu katibu mkuu wa CCM bara Mwigulu Nchemba akiwahutubia  wananchi wa  jimbo la Iringa mjini.

Wananchi  wa  jimbo la Iringa mjini wakimsikiliza Nchemba katika mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa Mwembetogwa.
 

Na Francis Godwin Blog
NAIBU katibu mkuu wa  chama cha mapinduzi (CCM) Bara Mwigulu Nchemba awahakikishia  wananchi wa jimbo la Iringa mjini kuwa  muda wa mbunge wa  jimbo hilo kuongoza umefika kikomo na kuwa ataongoza mapambano ya kumng’oa mwakani katika uchaguzi mkuu.

Akiwahutubia  wananchi  wa jimbo la Iringa mjini leo katika uwanja wa Mwembetogwa Nchemba ambae ni naibu  waziri wa fedha  alisema  kuwa mbali ya mbunge  huyo kupewa nafasi hiyo ya bure mwaka 2010 ila bado ameshindwa  kuwa na huruma na wananchi wa  jimbo hilo na kuendelea kujinufaisha yeye badala ya kuwekeza kwa  wananchi hasa  vijana na ndio  sababu ya kushindwa kufanya vikao na wanachama wake na kuendelea kuitisha maandamano badala ya kufanya kazi.

“Tutajipanga  vema kila kona ya jimbo la Iringa mjini ili kulirudisha jimbo mikononi mwa CCM kwa  kumpata mbunge ambae  atawatumikia  wananchi na sio wa kujitumikia yeye na kuwa mbunge wa maandamano kwa kipindi chake  chote”

Nchemba  alisema  kuwa kutokana na kazi  kubwa iliyopfanywa na vijana wa jimbo la Iringa kwa kumpigania mbunge Msigwa alipaswa  kuwa na roho ya huruma kwa vijana hao ikiwa ni pamoja na kuwageuza daraja na kuwafanyisha maandamano yasiyo kwisha badala ya kuwaanzishia miradi ya kiuchumi.

“Hivi tazameni leo maeneo  yote ya makanda wa Chadema majimboni mwao ni maandamano kila siku kila wakati utasikia hakuna kulala makamanda huku mbunge anashindwa kuwasaidia …..na siku hizi wanakuja na hoja  ya makamanda pambaneni tutachukua nchi huku hata kata kwao ni ndoto  sasa niwaambie  leo hata nusu ya nchi hii kamwe  hawatapata”

Asema  mmoja kati ya mke wa  kiongozi mojawapo wa Chadema alimuuliza hivi kwa nini mume wake anapenda  sana maandamano alimjibu  kuwa mume  wake  huyo akichukia huwa anafanya maandamano ndani ya chumba cha  kulala.
Nchemba  pia ameponmgeza  utendaji kazi wa mbunge wa  viti maalum mkoa wa Iringa Ritta Kabati na kuwa  siku  zote  amekuwa akiwapigania wananchi wa jimbo la Iringa mjini bungeni tofauti na mbunge wa jimbo mchungaji Msigwa ambae amekuwa akiongoza kwa kufanya maandamano.

Katika hatua  nyingine Nchemba  alisema amesema kuwa muda wa matajiri kuendelea  kujinufaisha na misamaha ya kodi  umekwisha na  kuwa anajipanga  kupeleka sheria bungeni itakayowabana wafanyabiashara wakubwa kulipa kodi kama  wanavyolipa wafanyabiashara  wadogo.

Alisema kuwa  watu  wanapata misamaha  hadi inakatisha tamaa kwani ni pesa nyingi za kimaendeleo zinapotea  kutokana na utitiri wa misamaha inayoendelea  kutolewa .

“Napeleka sheria katika bunge  hili la bajeti itakayofuta misamaha ya kodi kwa viwanda na wafanyabiashara  wakubwa…inakuweje  wananchi masikiti hata  wanapotaka kuanzisha  saluni wanalipizwa kodi ila wafanyabiashara  wakubwa na baadhi ya  watu pia nitapeleka sheria ya kubana matumizi ya  fedha za umma”

Alisema kuwa inashangaza  kuona mashirika ya umma yanavuna na kutumia huku wanyonge wakiendelea  kuteseka na walimu na askari  wakiendelea kukosa kulipwa madai yao.

“hatuwezi  kusema  leo  walimu ama  askari ni wengi  wakati watu  wanakwepa  kulipa kodi huku  wanafunzi  wakikosa mikopo ya elimu ya juu eti kutokana na kukosa fedha  wakati watu  wengine  wanakwepa kodi….hili ni jambo la aibu sana najua  wapo wabunge  watakaopinga ila  wananchi mtaona ni nani ni mbunge wa  wananchi …kwani najua wapo  wabunge ambao hawalipendi hili watapinga ila lazima nilifikishe hata kama chungu ila lazima suala hili likomeshwe”.

Chapisha Maoni

0 Maoni