Na Denis Mlowe, Ismani
MFUKO
wa Hifadhi ya Misitu Tanzania (TaFF) kwa kushirikiana na Mtandao wa
Jamii wa Usimamizi wa Misitu Kanda ya Kitapilimwa (MJUMIKK) umewakabidhi
mashine sita za kukamua asali na mizinga ishirini kwa vikundi vya
ujasiriamali vinavyojishughulisha na ulinaji wa asali katika kata za
Kitapilimwa na Kiwele katika jimbo la Ismani mkoani Iringa
Akizungumza
wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika kijiji cha
Kinywang’anga hivi karibuni, katibu wa mtandano wa MJUMIKK, Samson Fuko
alisema lengo la msaada huo ni kuleta ufanisi wa kulinda, kutunza na
kutumia kwa njia endelevu rasilimali za misitu na kuongeza kipato cha
mwananchi mjasiriamali.
Alisema
mashine hizo zitakuwa shamba darasa la ufugaji wa nyuki na upandaji
miti utakaotumika kutoa mafunzo kwa vitendo kwa wanachama wake na kutoa
elimu kwa jamii juu ya uhifadhi wa mazingira.
Fuko
alisema mtandao huo umefanikiwa kuongeza idadi ya wanachama kutoka 50
waliokuwa mwanzao hadi wanachama 200 walioko sasa ambao unajihusisha na
ufugaji wa nyuki unaotekelezwa katika vijiji sita kati ya vijiji 11.
Alivitaja
vikundi vilifaidika na msaada huo kuwa ni Kinywang’anga, Faraja group,
Twiga group, Mshikamano. Jitegemee na kikundi cha Umoja vyote
vikipatiwa mizinga mashine na za kukamulia asali pamoja na mavazi
maalumu ya kuvaa wakati wa kulina asali vyote vikiwa na thamani ya sh.
milioni 4.5
Aidha
aliwataka wadau kuvisaidia vikundi vya ufugaji nyuki mizinga ya nyuki
na mbegu za miti kwa lengo la kuanzisha shamba darasa la ufugaji wa
nyuki na shamba darasa la upandaji miti na mavazi ya kuvunia asali kwa
vikundi hivyo.
Kwa
upande wake mgeni rasmi Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa
Iringa Jesca Msambatavangu aliyekuwa mgeni rasmi katika makabidhiano ya
mashine hizo amewaasa wazazi na walezi kuwahamasisha vijana kujiunga
katika shughuli za maendeleo wasiwaache wakilegalega kwani vijana hao
ndio nguvu kazi ya taifa
Alisema
maendeleo ya mtu hayaletwi kwa kukaa bila kujishughulisha na kukaa
vijiweni na kuwataka wajasiliamali hao kutumia fursa waliyoipata
kuitumia katika kujiletea maendeleo yao na taifa kwa ujumla.
Aidha
Msambatavangu aliwahidi wafugaji nyuki kuwatafutia soko la bidhaa zao
kuweza kuwafikia watu wengi zaidi katika jamii ya mkoa wa Iringa na nje
ya nchi.
Msambataangu
ambae pia ni mlezi wa vikundi hvyo amewaeleza wananchi kuwa kiongozi
bora ni yule anaetekeleza majukumu aliyopewa na wananchi na sio
kuwadharau wale waliompa dhamana ya kuwa kiongozi
Msambatavangu
amewataka viongozi wote waliopewa dhamana na wananchi kuwatumikia na
kuwatatulia matatizo yao mda wowote wanapowahitaji na kuwajibika sio
kukaa na kutoa lawama.
Aidha
amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Pudensiana
Kisaka kwa kazi anayofanya ikiwa ni moja ya utekelezaji wa
majukukumu aliyopewa na serikali na amesema kuwa kiongozi huyo anapaswa
kuigwa na viongozi wa halimashauri nyingine kwani amekuwa akisikiliza
matatizo ya wananchi katika halimashauri yake na kuyafanyia kazi.
0 Maoni