Kamimu
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Afya NHIF Khamis Mdee akizungumza na
wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari kwenye hoteli ya Oceanic Bay
mjini Bagamoyo asubuhi hii wakati wa seina inayojadili masuala
mbalimbali yakiwemo mafanikio ya mfuko huo, malengo na Changamoto zake
katika kufanikisha huduma ya afya kwa jamii, ambapo uwigo wa walengwa
katika huduma hizo umeongezeka kutoka kaya 120 mwaka 2009 na kufikia
kaya 668.474 mwaka 2014 sawa na wanufaika milioni 4.01 na mpaka sasa
mfuko huo unafanya kazi na Halmashauri za wilaya 129 katika nchi nzima
kati ya Halmashauri 168 zilizopo lakini pia tayari Halmashauri 20 kati
ya hizo zimeshahamasishwa na zitaingia katika mpango huo siyo muda
mrefu, .(PICHA NA KIKOSIKZI CHA FULLSHANGWE-BAGAMOYO)
Eugen
Mikongoti Mkurugenzi wa Uendeshaji akitoa mada katika semina hiyo juu ya
uchangiaji wa huduma za mfuko wa bima ya afya kulia ni Raphael Mwamoto
Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti na katikati ni Rehani Athman Kaimu
Mkurugenzi wa \mfuko wa afya ya Jamii (CHF)(P.T)
Dk Frank
Lekey Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Kitaaluma akitoa mada kuhusu
uboreshaji wa huduma za mfuko wa Afya ya jamii ambapo kwa sasa wanafanya
kazi na hospitali za serikali na baadhi ya hospitali za mashirika ya
dini.
Rehani
Athman Kaimu Mkurugenzi wa \mfuko wa afya ya Jamii (CHF) akizungumzia
mafanikio yaliyokwishapatikana kutokana na huduma za mfuko wa Afya ya
jamii
John
Bwire Mkurugenzi wa kampuni ya Raia Mwema na baadhi ya wahariri wa
vyombo vya habari wakifuatilia mada mbalimbalzinazotolewa katika semina
hiyo
Kulia ni Mhariri Dany Mwaijega na wenzake wakifuatilia majadiliano ya semina hiyo
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri na Mhariri mtendaji wa New Habari Bw. Absalom Kibanda akizungumza katika semina hiyo inayofanyika mjini Bagamoyo anayefuata ni Abdalla Majura kutoka ABM Radio.
Mhariri wa Gazeti la Mawio Jabir Idrissa akitoa mchango wake wakati wa majadiliano katika semina hiyo
Kamimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Afya NHIF Khamis Mdee na viongozi wengine wa mfuko huo wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufunguliwa rasmi mjini Bagamoyo.
Wahariri mbalimbali wakibadilishana mawazo mara baada ya kufungua semina hiyo
0 Maoni