Unordered List


VIONGOZI WA TAWI LA CCM SAUT MWANZA WATATHIMINI MIAKA NANE TOKA KUAZISHWA KWAO


Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na wanachama wa CCM Tawi la SAUT Kambarage ambapo aliwaambia kuwa wasomi wa vyuo wanatakiwa kuchangia mawazo yao kwenye chama ambayo yatasaidia kuleta mabadiliko hasa ya kiuchumi ,alisema ni vyema kuja na mikakati ya kuonyesha uchumi umepanda kwa mwananchi kuliko huu wa sasa ambao unaonyesha uchumi umepanda lakini ni uchumi wa kwenye makaratasi.Uongozi Tawi la SAUT Kambarage ulimualika Katibu wa Itikadi na Uenezi kuja kushuhudia makabidhiano ya Uongozi na tathmini ya Tawi kwa miaka minane sasa.
 Aliyekuwa Rais wa Serikali ya Wanafunzi katika Chuo cha SAUT Mwanza Ndugu Dova Mcheshi akizungumza wakati wa shughuli ya kukabidhiana Uongozi wa Tawi la SAUT Kambarage ambapo aliwaambia wanachama wa CCM katika Chuo cha SAUT kuwa kuanzia sasa chama kinajiimarisha zaidi kwenye Chuo cha SAUT.Dova laiyekuwa CHADEMA lakini sasa amejiunga na CCM .
 Wadada wakiwa wamependeza na Sare yao ya Chama.
 Viongozi wa CCM mkoani Mwanza na Viongozi wa Serikali ya wanafunzi wakiwa kwenye picha ya pamoja na Katibu Mwenezi wa CCM Taifa Ndugu Nape Nnauye.
 Wanachama wa Tawi la CCM SAUT Kambarage,Mwanza.

Chapisha Maoni

0 Maoni