Unordered List


WAZIRI: TUWAEPUSHE VIJANA WETU NA UHAFIDHINA


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon,  akifunguza majadiliano  kuhusu mazingira yanayochangia kuendenea kwa vitendo vya  kigaidi.  majadiliano hayo yamefanyika siku ya  Jumatano yakitangulia mkutano wa nne utakafanya tathmini kuhusu Mkakati wa Umoja wa Mataifa wa Kudhibidi Ugaidi.  Katika salamu zake, Katibu Mkuu amesema hakuna sababu iwayo yoyote ile  inayoweza kuhalalisha ugaidi.  Kulia kwake ni Rais wa Baraza  Kuu la Umoja wa Mataifa Bw, John Ashe .
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe.  Pereira Silima ( Mb) akichangia majadiliano hayo. Naibu  Waziri anaongoza ujumbe wa Tanzania.  Katika  mchango wake amesema kuna kila sababu ya  kuhakikisha kuwa vijana hasa wale wasiokuwa na  ajira hawashawishiki kujiunga na uhafidhina na kwamba kutoka na changamoto mbalimbali zikiwamo za ukubwa wa mipaka baina ya nchi na nchi, tishio la ugaidi na uhafidhina kwa nchi za Afrika Mashariki ni kubwa.
Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huu  ukiongozwa na Naibu Waziri Silima walioketi  nyuma ni  Bw.  Abdalla Khamis  Afisa katika Uwakilishi wa Kudumu na    Bw. David Hiza. Kamishna Msaidizi wa  Jeshi la Polisi na  Mratibu  Kituo cha Kitaifa cha  Kuratibu Mapambano dhidi ya Ugaidi.
Wajumbe ukumbini

Chapisha Maoni

0 Maoni