Unordered List


KINANA AMALIZA ZIARA YAKE KOROGWE



 Katibu  Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishona nguo kwenye ofisi ya Veronica Simba (kushoto) iliyopo Mombo Sokoni,kulia ni Mbunge wa Korogwe Vijijini Ndugu Stephen Ngonyani ,Katibu Mkuu alikuwa kwenye ziara ya siku moja katika wilaya ya Korogwe Vijijini ambapo licha ya kukagua miradi mbali mbali ya ujenzi wa maabara na ofisi za CCM alipata nafasi ya kuwahutubia wananchi na kuwasikiliza  .

  Katibu  Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimuelekeza Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kushona nguo kwenye ofisi ya Veronica Simba (kushoto) iliyopo Mombo Sokoni.
 
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Ueneziwakinunua matunda kabla ya kwenda kwenye mkutano wa hadhara Mombo.


 Diwani wa kata ya Mombo akishangiia baada ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kutamka wazi kuwa katika kuhakikisha wanapata halmashauri ya mji mdogo.
 Mama akiwa amembeba mwana ili awaone viongozi wake vizuri kwenye uwanja wa mikutano Mombo ambapo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alihutubia.
 Wananchi wakiwa wamekaa kwa shauku ya kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCm Ndugu Abdulrahan Kinana.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kulia) akiwapungia watu wakati wa kuwasili kwenye uwanja wa mikutano mjini Mombo akiwa pamoja  na Katibu wa NEC Itikadi Nape Nnauye
 Katibu Mkuu akiwapugia watu waliojazana kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Mombo
 Umati wa wakazi wa Mombo uliojitokeza kwenye Mkutano wa Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Mombo ambapo aliwaambia wananchi hao wanachofanya wapinzani ni biashara, kwani kwao kuandamanisha watu ni mtaji mzuri wa kuwaingizia pesa kutoka nje.

 Umati wa watu ukimsikiliza Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na na Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Tanga Aisha Kigoda pamoja na Mjumbe wa NEC wilaya ya Korogwe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi mkoani Tanga Dk. Edmund Mdolwa wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Mombo.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Mombo.
Wananchi wakifuatilia mkutano wa Kinana mjini Mbombo
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa amekaa kwenye kiti tayari kupokea zawadi kutoka kwa wamasai wanaoishi Mombo.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokea zawadi kutoka kwa wamasai wa Mombo.
 Katibu wa CCM Ndugu Abdulrahman akipeana mkono wa shukrani kwa kiongozi wa wamasai wa Mbombo Samng'o Maikaambaye [ia ni mwenyekiti wa Tawi la Chang'ombe ,Mombo. na Sufyan Omar



Chapisha Maoni

0 Maoni