Unordered List


MWENYEKITI WA UVCCM MKOA WA ARUSHA AZINDUA MRADI WA MAJI SAFI NA MAJI TAKA

Wao wakiendelea kupanga maandano wengine wanaendelea na kazi za Chama ndani ya ummani ili baadae tuwe na cha kuwaeleza tukiwa tunawaomba ridhaa kwa mara nyingine manake si rahisi Watanzania wa sasa wakupe kura eti kwa kuwashawishi kuwa mliendesha migomo na maandamano Nchi nzima maandamano ambayo ndugu zao wasio na hatia wengine wamekufa na wengine kujeruhiwa vibaya.
Ila utakapo waambia Watanzania kuwa Shule zimejengwa, Zahanati zimeongezwa, Barabara zimejengwa, Umeme umeongezeka kwenye gridi ya Taifa, Amani ya Taifa letu tutaendelea kuitetea hapo watakuelewa manake ndicho wanachotaka kusikia kwa sasa kuandamana wameandamana na madhara wameyaona.
Picha ni jana katika Uzinduzi wa Mradi wa Maji Safi na Maji Taka Kata ya Unga Ltd. Mwendelezo wa utekelezwaji wa Ilani ya CCM 2010 inayoitaka Serikali miradi ya Maji kufikia 70% Mijini na 60% Vijijini..... Kazi nzuri iliyofanywa na kusimamiwa na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa pamoja na Mhe. Diwani wakishirikiana na Wananchi.
CCM Oyeeee........
Kidumu Chama Cha Mapinduzi....





By Sufyan Omar

Chapisha Maoni

0 Maoni