Wao wakiendelea kupanga maandano wengine wanaendelea na kazi za Chama
ndani ya ummani ili baadae tuwe na cha kuwaeleza tukiwa tunawaomba
ridhaa kwa mara nyingine manake si rahisi Watanzania wa sasa wakupe kura
eti kwa kuwashawishi kuwa mliendesha migomo na maandamano Nchi nzima
maandamano ambayo ndugu zao wasio na hatia wengine wamekufa na wengine
kujeruhiwa vibaya.
Ila utakapo waambia Watanzania kuwa Shule zimejengwa, Zahanati zimeongezwa, Barabara zimejengwa, Umeme umeongezeka
kwenye gridi ya Taifa, Amani ya Taifa letu tutaendelea kuitetea hapo
watakuelewa manake ndicho wanachotaka kusikia kwa sasa kuandamana
wameandamana na madhara wameyaona.
Picha ni jana katika Uzinduzi wa Mradi wa Maji Safi na Maji Taka Kata
ya Unga Ltd. Mwendelezo wa utekelezwaji wa Ilani ya CCM 2010 inayoitaka
Serikali miradi ya Maji kufikia 70% Mijini na 60% Vijijini..... Kazi
nzuri iliyofanywa na kusimamiwa na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa pamoja
na Mhe. Diwani wakishirikiana na Wananchi.
CCM Oyeeee........ Kidumu Chama Cha Mapinduzi....
|
0 Maoni