Diamond asalimisha magwanda polisi
MSANII wa
muziki wa kizazi kipya, Naseeb Abdul 'Diamond', amekiri kuhojiwa na
polisi baada ya kukutwa na hatia ya kuvaa mavazi yanayoaminika kuwa ni
sare (magwanda) ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Hata
msanii huyo alidai kwamba mavazi hayo hayakuwa sare za jeshi hilo na
kwamba yeye aliyanunua alipokuwa Ujerumani ingawa baada ya kuhojiwa
aliyasalimisha.
Diamond
alipanda jukwaani Jumamosi iliyopita katika onyesho la Fiesta jijini Dar
es Salaam akiwa na mavazi hayo jambo ambalo liliibua mjadala.
Akizungumza
jana Alhamisi, Diamond alikiri kupata ujumbe uliomtaka kufika Kituo cha
Oysterbay, Dar es Salaam na madansa wake akiwa na nguo hizo.(P.T)
"Awali
Meneja wangu alishikiliwa kwa muda na mimi nikatakiwa kufika na zile
nguo nikiwa na madansa wangu ambao pia walizivaa, nilifanya hivyo na
kuziacha nguo baada ya taratibu zote za kisheria kukamilika," alisema.
"Nisingeweza
kukaidi amri ya dola, nilifika na yale mavazi na nikahojiwa kwa saa
kadhaa. Nikaeleza kwamba yalikuwa yakifanana tu na ya jeshi na hayakuwa
sare rasmi za jeshi, kikubwa nilihitaji kumaliza tatizo," alisema.
Diamond
alifafanua pia kwamba si kweli kwamba alichukuliwa dhamana na Chief
Kiumbe, ukweli ni kwamba alisindikizwa na mdau huyo wa sanaa kama kaka
tu kutokana woga aliokuwa nao, lakini hakushikiliwa na kutakiwa kutoa
dhamana yoyote.
Chanzo:Mwanaspoti
0 Maoni