OFISI YA WAZIRI MKUU YAFANYA TATHMINI YA HALI YA CHAKULA NA LISHE MKOANI SIMIYU
Bw.
Clement Ngosha wa kijijini Kabita Wilayani Busega, Simiyu, akitumia
mbegu za mahindi kueleza hali ya chakula kijijini hapo kwa wataalam wa
Tathmini ya Hali ya Chakula na Lishe inayofanywa na Ofisi ya Waziri
Mkuu, Oktoba, 2014.
Mtaalam
wa Usalama wa chakula kutoka Wizara ya kilimo, chakula na Ushirika, Bi.
Tatu Kayumbu akiihoji moja ya kaya kijijini Mwamanyili,Wilayani Busega,
Simiyu wakati wa Tathmini ya Hali ya Chakula na Lishe inayofanywa na
Ofisi ya Waziri Mkuu kijijini hapo, Oktoba, 2014.
Baadhi ya
wanakijiji wa kijiji cha Kabita wilayani Busega, Simiyu wakifuatilia
mkutano wa kijiji uliokuwa ukijadili hali ya Chakula na Lishe kijijini
hapo wakati Ofisi ya Waziri Mkuu ilipofika kijijini hapo kufanya
tathmini ya masuala hayo Oktoba, 2014.(P.T)
Na. Ibrahim Hamidu
Ofisi ya
Waziri Mkuu kupitia Idara ya Uratibu wa maafa inafanya Tathmini ya Hali
ya Chakula na Lishe Mkoani Simiyu katika Wilaya zake zote ambazo ni;
Halmashauri za Wilaya za Bariadi, Itilima, Maswa ,Bariadi Mji, Meatu na
Busega.
Akiongea
mkoani Simiyu kiongozi wa Wataalam wa tathmini ambaye pia ni mratibu wa
shughuli za maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Edgar Senga alibainisha kuwa
Ofisi ya Waziri Mkuu imefikia maamuzi hayo ya kufanya tathmini mkoani
Simiyu baada ya mkoa huo kutuma maombi katika Ofisi hiyo kuwa wana
upungufu wa chakula.
" Ofisi
ya mkoa ya Simiyu ilileta maombi kwa ofisi ya Waziri Mkuu kuwa
wanaoupungufu wa chakula takribani tani 48,975, kwa kuwa Ofisi yetu ndio
yenye dhamana ya kuratibu misaada ya chakula hivyo haikuwanabudi
kufanya tathmini ya haraka ili kubaini hali ya chakula ya mkoa huu ili
kuweza kuamua namna ya kushughulikia maombi yao ya msaada wa chakula"
alisema Senga
Senga
alibainisha kuwa Wataalam wa tathimini hiyo wanatoka Wizara ya Kilimo,
Chakula na Ushirika katika Idara ya Usalama wa Chakula ambao kwa
kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu wametawanyika katika Wilaya zote za
Mkoa wa Simiyu ambapo katika kila Wilaya vitachaguliwa vijiji vitatu
vya kufanyiwa tathmini.
"Katika
kila kijiji wataalamu hawa watakuwa wanamadodoso ya Wilaya na kijiji
ambayo yatasaidia kutoa taarifa mahsusi za hali ya chakula na Lishe
katika ngazi ya Wilaya na Kijiji, lakini pia wataalamu wanayo madodoso
ya kaya ambayo yanalenga kupata taarifa za hali ya chakula na Lishe kwa
kaya husika kwa vijiji vitakavyoteuliwa na Serikali za vijiji hivyo. Kwa
kuzingatia kuwa wataalam wa masual ya chakula katika ngazi ya Wilaya
watakuwa wanahusishwa ninaamini tutapata taarifa bora ya hali ya chakula
ya mkoa wa Simiyu " alisisitiza Senga.
Akiongea
Ofisini kwake alipotembelewa na ujumbe wa Wataalamu hao Katibu Tawala
Msaidizi (Uchumi na Uzalishaji) mkoani Simiyu, Bw. Joseph Nandira
alibainisha kuwa Katika kipindi cha msimu wa 2013/2014, Mkoa ulijiwekea
malengo ya kuzalisha jumla ya tani 1,003,578za mazao ya chakula aina ya
nafaka/wanga na tani 150,257aina ya mikunde. Mavuno halisi
yaliyopatikana ni tani 476,024 za chakula aina ya nafaka/wanga na tani
74,944 za chakula aina ya mikunde.
Nandira
alibainisha kuwa kutokana na tabia ya wananchi kuuza sehemu kubwa ya
chakula ili kukidhi mahitaji ya familia zao, tathmini ya hali ya chakula
tuliyoifanya mwezi Julai 2014, tulibaini kuwa Mkoa Unaupungufu wa
chakula wa tani 48,975 za nafaka ambao umeanza kuanzia mwezi Oktoba na
upungufu huo wa chakula unatarjiwa kuwepo mwezi Novemba/Desemba hadi
Februari, 2015 kama wilaya hazitapata msaada wa chakula.
"Tathmini
hiyo ilibaini Halmashauri za Wilaya za Busega na Meatu zina upungufu wa
chakula kuanzia mwezi Agosti, 2014 hadi Februari, 2015. Halmashauri za
Wilaya za Bariadi, Itilima, Maswa na Bariadi Mji zina upungufu wa
chakula kuanzia mwezi Oktoba, 2014 hadi mwezi Februari, 2015. Ili
kukidhi haja ya upungufu wa chakula ndio maana tuliomba jumla ya tani
48,975 kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu." Alisema Nandira
Nandira
alifafanua kuwa ili kuhakikisha tatizo la upungufu wa chakula linakwisha
tayari mkoa unayomikakati ambayo inajikita katika Kuwahimiza wananchi
kutumia vizuri chakula kilichopatikana na kuepuka matumizi yasiyo ya
lazima. Kutoa elimu kwa wananchi kuhusu makadirio ya mahitaji ya chakula
ngazi ya kaya kwa mwakapamoja na Kuwashauri wananchi kuuza sehemu ya
mifugo yao na kujinunulia chakula wakati huu ambapo chakula bado kina
bei ndogo na kinapatikana ndani ya Wilaya na Mkoa.
Aliongeza
kuwa mkoa unaendelea kuwashauri wananchi kujinunulia chakula kutokana
na fedha za mauzo ya pamba. Kutoa elimu kwa wananchi kuhusu hifadhi bora
ya chakula, ikiwa ni pamoja na matumizi ya vihenge bora/vya kisasa na
madawa ili chakula kisibunguliwe na wadudu. Kuwashauri wananchi kuuza
ziada ya chakula walichovuna na si vinginevyo.
Kwa
mujibu wa sensa ya watu ya mwaka 2012 mkoa wa Simiyu una jumla ya watu
1,584,157 ambao wanahitaji jumla ya tani 404,752 za chakula aina ya
nafaka/wanga na tani 144,553 za chakula aina ya mikunde kwa kipindi cha
msimu wa mwaka 2013/2014.
0 Maoni