katibu mkuu wa umoja wa vijana wa ccm ndugu SIXTUS MAPUNDA leo kwa kushirikiana na mkuu wa wilaya ya
korogwe Mh Mrisho Gambo na mbunge wa korogwe vijijini Prof Majimarefu wameezeka maabara moja na kumimina zege la lenta katika maabara
ya pili kwa ushirikiano mkubwa na wananchi wa korogwe
awali kulikuwapo na taarifa kuwa Halima mdee angekuwa na
mkutano mombo lakini baadae uliahirishwa baada ya kusikiwa kuwa sixtus angeenda
kuezeka maabara pia mombo,wapashaji wanasema mdee alistuliwa kuwa kwa mazingira
ya mombo sasa watu wangeenda kwenye tukio la kujenga maabara zaidi kuliko kuja
kwenye mkutano wa hadhara hivyo wakamsihi asogeze mbele mkutano wake jambo
ambalo alilifanya.
sixtus mapunda amekabidhi mabati 450 kwa wilaya ya korogwe
vijijini.na baadhi ya vitendea kazi vingine vingi
huu ni muendelezo wa ziara za katibu mkuu wa uvccm mara baada ya kumalizika
kwa baraza kuu la vijana Nov 9 ambapo
alishakagua ofisi ya uvccm mkoa wa Arusha na Kilimanjaro na sasa yupo Tanga
akizungumza katika mkutano wa hadhara ktk kata ya Hale
korogwe , sixtus alisema;
“…VIJANA WENZANGU NA WASIHI SANA KUENDELEA KUILINDA AMANI
YETU NA KUSHIRIKIANA NA VIONGOZI WETU KATIKA KUJILETEA MAENDELEO
MNAJUA KUNAWATU WALE KAZI YAO NI MANENO TU,CCM KAZI
YAKE NI KUTENDA,NAWAOMBA PIA MJITAHIDI
KUISOMA KATIBA MPYA NA KUIPIGIA KURA YA ‘NDIO’ HAPO APRIL30 KWAKUWA NI KATIBA YENYE MAMBO MAZURI KWA
WATANZANIA,NI KATIBA INAYOLINDA ARDHI YETU,MALIASILI ZETU,IMETUPA BARAZA LETU
VIJANA,IMETOA HAKI KWA WANAWAKE NA MAMBO MENGINE MENGI,NI MUHIMU KUACHA
KUSIKILIZA RADIO MBAO,TUISOME WENYEWE
NAWAOMBA TUENDELEE NA MOYO WA KUCHANGIA MAENDELEO YETU KAMA
AMBAVYO MNASHIRIKIANA NA MBUNGE WENU NA MKUU WA WILAYA YENU,JUU YA KUPATIWA
BIMA YA AFYA NA KUJENGA MAABARA,SISI TUPO NA TUTAENDELEA KUSAIDIANA KWA HALI NA
MALI..”
0 Maoni