MSHAMBULIAJI
wa Yanga, Mrisho Ngassa amepata zali Afrika, baada ya kumaliza kinara
wa mabao kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, licha ya klabu yake kuaga
mashindano hayo alfajiri kabisa.
Ngassa
amemaliza kinara baada ya kufunga mabao sita na kufungana na Ndombe
Mubele wa AS Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Haythem
Jouini wa Esperance de Tunis ya Tunisia na El Hedi Belameiri wa ES Setif
ya Algeria.
Ni baada
ya Ligi ya Mabingwa Afrika kufikia tamati wikiendi iliyopita na ES Setif
kutangazwa mabingwa wapya wakibebwa na bao la ugenini kutokana na
matokeo ya sare bao 1-1 mchezo wa Algeria na sare mabao 2-2 mchezo
uliochezwa Kinshasa.
Ngassa
aliyafunga mabao hayo katika raundi ya kwanza walipocheza na Komorozine
ya Comoro mchezo wa kwanza walishinda 7-0 na marudiano walitoka kifua
mbele kwa mabao 5-2.
Yanga
ilitolewa kwenye mashindano na Al Ahly ya Misri kwa penalti 3-4. Lakini
Ngassa hawezi kupewa zawadi yoyote kwavile wamefungana na kiutaratibu
hata mchezaji akishinda tuzo hiyo CAF huitoa kwa klabu yake.
Chanzo:Mwanaspoti
0 Maoni