Unordered List


VIONGOZI WA SPLM KUTOKA SUDANI KUSINI WAMFUATA KINANA MASASI

 Jenerali James Kok ambaye ni Mjumbe wa kamati kuu, SPLM, Mbunge , amewahi kuwa Waziri wa masuala ya kijamiii na bisahara katika serikali ya umoja wa kitaifa  Sudan,SPLM - IG akiwasalimu wananchi wa Masasi. Msafara wa viongozi hao kutoka Sudani kusini ulifika wilayani Masasi kwa lengo la kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (mwenye shati la kijani) pamoja na viongozi wa chama cha SPLM kutoka Sudani Kusini wakiwa wameinua mikono juu kama ishara ya umoja na mshikamano,Masasi mkoani Mtwara.
Kutoka Kushoto ni Dkt. Cirino Hiteng,Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ,Bw.Goy Jooyul na Jenerali James Kok.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye mazungumzo na viongozi wa chama cha SPLM kutoka Sudani ya kusini waliomfuata Masasi mkoani Mtwara ambapo Katibu Mkuu wa CCM yupo kwenye ziara ya kukijenga na kukiimarisha chama mkoani Mtwara.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza  Jenerali James Kok kutoka chama cha SPLM Sudani ya Kusini ambaye yeye pamoja na viongozi wenzake wamefika mpaka Masasi kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa CCM.

Chapisha Maoni

0 Maoni