Katibu
Mkuu wa Jumuiya ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) na mjumbe wa
Halmashauri Kuu ya Taifa (M-NEC) Ndugu Sixtus Mapunda amesema kuwa
Chadema wamepanga njama haramu za kuvuruga uchaguzi wa Serikali za mitaa
kwa kuwaandaa vijana wa kufanya vurugu na kuwazuia akina mama na wazee
wasiende katika maeneo ya kupigia kura.
Mapunda
ameyasema hayo leo majira ya saa tano na nusu asubuhi wakati
akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mwanzugi Kata ya Igunga , mkoani
Tabora ambako yupo katika ziara ya Kikazi ya siku kumi na nne katika
mikoa ya Tabora, Shinyanga, Geita na Kagera.
“..tumepata
taarifa za kuaminika kuwa Chadema wameandaa vijana na kuwaandalia
viroba na bangi ili waweze kufanya vurugu siku ya uchaguzi na kuwazuia
wananchi kwenda kupiga kura katika vituo vilivyoandaliwa.,tunawataka
waache mpango huo mara moja kwani vyombo vya dola viko macho na
vitawachukulia hatua wote watakaofanya hujuma hizo..”
alisema
Mapunda katika mkutano wa hadhara uliofanyika eneo la Mwanzugi stendi
na kuhudhuriwa na mamia ya wakazi wa kijiji cha Mwanzugi.
Pia,
Mapunda amewataka wananchi kuwachagua Viongozi wanaotokana na Chama Cha
Mapinduzi kwani ni waaminifu, wakweli na wenye anuani kamili kwa maana
ya kuwa wanazo ofisi zinazotambulika katika kila kijiji na Kata ambako
wananchi wanaweza kupeleka malalamiko yao na kusikilizwa tofauti na
vyama vingine ambavyo havina ofisi wala anuani ya Kudumu.
Mapunda
ameendelea na mikutano yake ya hadhara katika Mkoa wa Tabora ambako
anatarajia kuzungumza na wananchi wa wilaya za Kaliua, Urambo na Nzega.
0 Maoni