Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Waziri wa Afya Rashid Seif Suleiman pamoja na Viongozi wengine alipofika katika Hospitali ya Mnanzi Mmoja leo kufungua jengo jipya ya upasuaji wa Ubongo na Uti wa Mgongo (Neurosurgical Unit) ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya miaka 51 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Mnanzi Mmoja Dk.Jamala Adam Taibu,alipofika kufungua jengo jipya ya upasuaji wa Ubongo na Uti wa Mgongo leo (Neurosurgical Unit) ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya miaka 51 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akikata utepe kufungua jengo jipya ya upasuaji wa Ubongo na Uti wa Mgongo (Neurosurgical Unit) katika Hospitali ya Mnanzi Mmoja leo (kushoto) Waziri wa Afya Rashid Seif Suleiman na Prof,Dk. Mahmoud Quresh Mwakili wa taasisi ya NDkutoka Spein sherehe hizo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya miaka 51 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kulia) akipata maelezo kutoka kwa Dk.Mohamed Ali Haji (ustadh) wa sehemu ya upasuaji wa Ubongo na Uti wa Mgongo (Neurosurgical Unit) katika Hospitali ya Mnanzi Mmoja wakati Rais alipowatembelea wagonjwa mbali mbali waliokwisha fanyiwa matibu na Kituo hicho baada ya kulifungua jengo hilo leo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya miaka 51 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pilikushoto) na Makamo wa Kwanza wa Rais maalim Seif Sharif Hamad wakipata maelezo kutoka kwa Prof,Dk. Mahmoud Quresh Mwakilishi wa taasisi ya ND kutoka Spain wakati alipotembelea mashine za upasuaji baada ya kulifungua jengo jipya ya upasuaji wa Ubongo na Uti wa Mgongo (Neurosurgical Unit) katika Hospitali ya Mnanzi Mmoja leo (kulia) Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali Dk.Jamala Adam Taibu pia sherehe hizo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya miaka 51 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,[Picha na Ikulu.]
Wanafunzi wa Chuo cha Sayansi ya Afya wakiwa mbele ya jengo lajipya ya upasuaji wa Ubongo na Uti wa Mgongo (Neurosurgical Unit)katika Hospitali ya Mnanzi Mmoja baada ya kufunguliwa rasmi leo naRais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein likiwa la horofa mbili na uwezo wa vitanda 30 pamoja na vyumba (2)viwili vya upasuaji,[Picha na Ikulu.]
…………………………………………………………………………………
Na Miza Kona – Maelezo
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohammed Shein amekemea tabia ya baadhi viongozi wa Taasisi kuwazuia wafanyakazi wake kujiendeleza kielimu kwa lengo la kuongeza ujuzi na kuleta ufanisi.
Hayo ameyasema Hospitali kuu ya Mnazi Mmoja katika ufunguzi wa Jengo la Upasuaji Vichwa maji na Uti wa Mgongo ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra za maadhimisho ya miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Amesema tabia hiyo haifai kwani inarejesha nyuma maendeleo ya wafanyakazi na kuanzisha majungu, fitna na uhasama katika taasisi kati ya wafanyakazi wa kawaida na viongozi wao.
Amefahamisha kuwa taaluma ndiyo inayopelekea ufanisi bora wa kazi na kuleta mabadiliko kwa kutoa huduma bora na uhakika na kujenga taifa lililo imara.
“Mabadiliko hayaji bila ya kuwa na taaluma hasa katika sekta ya Afya hivyo viongozi waruhusuni wafanyakzi wenu kupata elimu ili waweze kufanyakazi kwa ufanisi”, alieleza Dkt. Shein.
Amesema lengo la Serikali ni kuipa hadhi Hospitali ya Mnazi Mmoja kuwa ya rufaa kwa lengo la kuimarisha huduma bora lakini kutokana upungufu wa vitendea kazi mabadiliko hayo yanakuja hatua kwa hatua.
Dkt. Shein ameeleza lengo la Serikali ni kutoa huduma bora za afya kwa wananchi kwa kutumia wataalamu wenye elimu na vifaa vya uhakika kadiri ya uwezo uliopo ili kuimarisha afya za wananchi.
Aidha Dkt Shein amesema jitihada kubwa zinahitajika katika kuandaa mipango madhubuti itakayosimamia kuendeleza kitengo cha upasuaji wa ubongo na uti wa mgongo kwa kutafuta wataalamu na madaktari bingwa watakaoendesha matibabu hayo.
Amesema kitengo cha huduma ya upasuaji wa ubongo na uti wa mgongo ni cha pekee kwa Afrika Mashariki na Kati ambacho kitasaidia kupnguza gharama za usafirishaji wa wagonjwa wa matatizo hayo nje ya nchi.
Amesisitiza madaktari kuwafanyia wagonjwa uchunguzi wa kina kabla ya kuwapa matibabu ili waweze kutoa huduma ya uhakika na kujiepusha kubahatisha.
Aidha ameutaka uongozi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja kukamilisha sheria na kuweka taratibu ili Hospitali hiyo iweze kujiendesha na kusimamia kazi bila kutegemea Serikali kuu
“Nijukumu la uongozi wa Hospitali hii kuandaa mipango mizuri itakayoweza kuiimarisha ili lengo la kujiendesha liweze kufanikiwa”. Alisitiza Rais wa Zanzibar.
Mapema akimkaribisha Mgeni rasmi, Waziri wa Afya Rashid Seif Suleiman alisema kupatikana kwa miundombinu katika kitengo hicho ni kuleta maendeleo katika sekta hiyo na ameeleza kitatoa huduma ya uhakika
Jengo hilo lenye vyumba viwili vya upasuaji, wodi nne za kulaza wagonjwa na chumba cha mikutano limejengwa kwa msaada wa Shirika moja la Hispania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na limegharimu zaidi ya shilingi Mill 600 ambapo asilimia 60 zimetolewa na wafadhili.
0 Maoni