Unordered List


RIDHIWANI KIKWETE AAHIDI KUTATUA TATIZO LA UMEME, MAJI KIWANGWA,CHALINZE

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete (kulia), akipata maelezo kutoka kwa Msimamizi wa ujenzi kutoka Kambi ya Mzinga ya JWTZ, Aloyce Mayunga (kushoto) alipokwenda kukagua ujenzi wa maabara ya Shule ya Sekondari ya Kiwangwa wakati wa ziara ya kikazi ya katika Kata ya Kiwangwa, wilayani Chalinze, Pwani leo.Aliwataka wajenzi hao kujenga maabara hayo kwa kuzingatia viwango. Katikati ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Bagamoyo, Saleh Mpimbwi.
 Ridhiwani Kikwete akizungumza na wakandarasi kutoka Kambi ya Mzinga ya JWTZ wanaojenga maabara ya Shule ya Sekondari ya Kiwangwa wakati wa ziara ya kuagua miradi ya maendeleo na kuwashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa mbunge miezi sita iliyopita. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Ridhiwani akinyoosha juu kadi ya Chadema aliyokabidhiwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa  Chadema Kijiji cha Masugulu ambaye amehamia CCM katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mwitemo Kata ya Kiwangwa leo
 Ridhiwani akihutubia wananchi  katika Kijiji cha Mwitemo
 Sehemu ya akina mama wakisikiliza kwa makini wakati Ridhiwani Kikwete akihutubia katika Kitongoji cha Magogoni, Kijiji cha Msinune, Kata ya Kiwangwa.
 Ridhiwani Kikwete akihutubia wananchi katika Kijiji cha Msinune, Kata ya Kiwangwa.
 Msanii kiongozi wa Kikundi cha sanaa cha Chanzala akifanya maajabu yake wakati mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Ridhiwani Kikwete katika Kata ya Kiwangwa

 Mwenyekiti mpya wa Serikali ya Kijiji cha Kiwangwa, Kata ya Kiwangwa, akifungua rasmi mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete katika Kata ya Kiwangwa ambapo pamoja na kusikiliza kero zao aliwashukuru wananchi kwa kumchagua mwaka jana.

 Mkazi wa Kiwangwa Shabani Dume akiuliza swali kwa kumtaka Mbunge Ridhiwani asaidie kuwepo dampo katika Kijiji cha Kiwangwa
 Kassim Makelele wa Kata ya Kiwangwa akimuomba Mbunge Ridhiwani kununua Ambulance kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Kiwangwa
 Diwani wa Viti Maalumu Tarafa ya Msata, Rehema Mno akielezea kwa wananchi jinsi alivyoshiriki kutatua kero za wananchi katika Kata ya Kiwangwa., 
 Ridhiwani akiteta jambo na Diwani wa Kata ya Kiwangwa, Yahaya Ramadhani  wakati wa mkutano huo
 Sehemu ya umati uliohudhuria katika mkutano huo
 Ridhiwani akihutubia katika mkutano huo ambapo aliwaambia viongozi wa Tanesco kuhakikisha wana peleka haraka umeme wa Wakala wa Umeme Vijijini (REA) katika Kijiji cha Kiwangwa
 Meneja wa Tanesco Wilaya ya Chalinze, Julius Doyi akiwaambia wananchi wa Kiwangwa kuwa umeme utaingia hapo mwezi huu.
 Meneja wa Mamlaka ya Usafi wa Maji Safi na Taka wa Chalinze,Injinia Christer Mchomba akielezea kwa wananchi mikakati mbalimbali ya kuharakisha upatikanaji wa maji katika Kata ya Kiwangwa.
 Ridhiwani akaimkabidhi Bondia Idd Pialali gloves 20 kwa ajili ya kuendeleza mchezo wa ngumi katika Kata ya Kiwangwa
Ridhiwani akimkabidhi mpira mmoja wa wa manahodha wa timu mbalimbali katika Kata ya Kiwangwa  kwa ajili ya kuendeleza soka katika kata hiyo.

Chapisha Maoni

0 Maoni