Unordered List


KINANA AFIKA NYUMBANI KWA MBOWE


Monday, March 23, 2015
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kuchimba msingi wa darasa katika shule ya msingi Modio,Masama Mashariki wilaya ya Hai.
Shule ya msingi Modio ilikumbwa na tetemeko la ardhi ambapo vyumba viwili vya madarasa,bwalo la chakula na ofisi ya walimu viliathirika.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili kitongoji cha Kiyungi kwenye daraja la MNEPO
 Daraja la linalounganisha wilaya ya Hai katika kijiji cha Mijungweni na wilaya ya Moshi vijijini katika kijiji cha Kiungi almaarufu kama daraja la MNEPO likiwa limekamilika kwa asilimia 90% ikiwa sehemu ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM mwaka 2010.

  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa kitongoji cha Kiyungi ambao daraja la MNEPO ni mkombozi wao.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupaka rangi kwenye bomba la daraja la MNEPO ikiwa sehemu ya kujenga na kuimarisha chama ambapo alitoa wito viongozi wawe mstari wa mbele  katika kazi za kuleta maendeleo kwa jamii.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipita kwenye daraja la MNEPO la Kiyungi la awali.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimia wananchi wa kijiji cha Kwasadala na kuwapa pongezi kwa kukipa chama cha CCM ushindi mkubwa kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Mtakuja.
 Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Leonidas Gama akisalimia wananchi wa kijiji cha Mtakuja
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwasalimu wananchi wa kijiji cha Mtakuja wilayani Hai.
 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro Ndugu Idd Juma akiwasalimia wakazi wa kijiji cha Mtakuja kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM kuhutubia wananchi hao.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Kijiji cha Mtakuja ambao walimsomea risala ya mgogoro wao na kiwanja cha Ndege cha KIA.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akivishwa vazi la Kimila la jamii ya wamaasai
 Wananchi wakiwa wamsindikiza  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mara baada ya kumaliza kuhutubia katika kijiji cha Mtakuja.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mganga Mfawidhi wa Wilaya ya Hai Dkt.Irine Haule .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza nje ya jengo la Mionzi la hospitali ya wilaya ya Hai ambapo aliwapongeza watumishi wa afya kwa kufanya kazi vizuri ya kutoa huduma kwa wananchi.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Waganga na Wauguzi wa Hospitali ya wilaya ya Hai.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa wilaya ya Hai na kuwaambia CCM imejipanga kurudisha majimbo yote yaliyopotea.
 Wananchi wakisikiliza kwa makini
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa wilaya ya Hai na kuwaambia CCM itakuwa makini katika kusimamia haki za wananchi
 Wananchi wakishangilia hotuba ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 Wananchi wakimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika Boma Ng'ombe.
Wasanii wa muziki wakizazi kipya wakitumbuiza mara baada ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kumaliza kuhutubia wananchi wa wilaya ya Hai.

Chapisha Maoni

0 Maoni