Unordered List


KINANA; ARUMERU MSIRUDIE MAKOSA



 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimu wananchi wa kata ya Shangarai waliojitokeza kumpokea na kumkaribisha katika wilaya ya Meru, jimbo la Arumeru Mashariki.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na kumshukuru na Kamanda wa Vijana CCM wilaya ya Arumeru Ndugu John Denielson Pallangyo kwa mchango wake wa kugharamia ujenzi wa msingi wa mochwari ya hospitali ya wilaya ya Tengeru.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Askofu Mkuu wa IEC Dkt. Eliud Issangya
 Jengo la Upasuaji mkubwa kama linavyoonekana kwa mbele.
 Bango la kumkaribisha Kinana kwenye shule aliyosoma  wakati huo ikiitwa West Meru Middle School.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimia wananchi kwenye uwanja wa Chuo cha Ualimu Patandi ,zamani West Meru middle school shule ambayo alisoma.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Shimbumbu Meru, wananchi ambao wanatatizo kubwa la maji kiasi cha kuamua kufanya biashara ya mawe ili wapate kubadilishana ama kununua maji.

Mama Maru Mungule akisoma risala kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana inayohusu matatizo ya maji yanayosababisha wananchi kufanya uharibifu mkubwa wa mazingira.
 Sehemu ya uharibifu wa mazingira unaofanywa na wananchi wa Kijiji cha Shimbumbu ambao inawalazimu kuuza mawe ili wapate maji .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa kijiji cha Shimbumbu ambao wamekuwa na shida ya muda mrefu ya maji,hata hivyo mhandisi wa maji wilaya ya Meru alisema zinahitajika shilingi milioni 120 kufikisha maji kwa wanakijiji hao.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa amekutana na Mzee Ezron Sumari waliesoma wote West Meru middle school.
Katibu Mkuu alikutana na mwanafunzi mwenzake huyo kwenye kijiji cha Shimbumbu, wilaya ya Meru.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akihutubia wananchi wa kijiji Singisi ambapo vijana 24 walijiunga na CCM wakitokea Chadema.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimkaribisha kwenye chama Nelson Kitomary aliyekuwa Katibu wa M4C Kanda ya Kaskazini
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na aliyekuwa MwenyekitiAmani Ole Silanga ambaye amejiunga na CCM rasmi leo kwenye mkutano uliofanyika Singisi wilayani Meru.


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata mapokezi makubwa katika kata ya Nkoanekoi
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mchungaji Kuvavenaeli Paniel Urio mara baada ya kuwasili katika kata ya Nkoanekoi.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali Mrisho Sarakikya mara baada ya kukutana katika kijiji cha Nkoanekoi  wilaya ya Meru
Katibu wa NEC Itikandi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali Mrisho Sarakikya mara baada ya kukutana katika kijiji cha Nkoanekoi  wilaya ya Meru

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa jengo la mashine ya kukobolea mpunga katika kijiji cha Lekitatu kata ya Usa River
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na vijana kwenda kwenye mutano wa hadhara.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kijiji cha Mbuguni
 Wananchi wa kijiji cha Mbuguni wakifuatilia mkutano
 Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Monduli Amani Ole Silanga akihutubia wananchi wa Mbuguni wilaya ya Meru.
 Katibu Mkuu wa CCM akitafakari jambo wakati mkutano ukiendelea.

  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa kijiji cha Mbuguni
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wazee wa kijiji cha Mbuguni mara baada ya kumaliza kuhutubia
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape akiwashukuru wananchi wa Mbuguni kwa zawadi ya mgolole.

Chapisha Maoni

0 Maoni