Unordered List


KINANA NDANI YA MKOA WA KILIMANJARO

.

KINANA AANZA ZIARA YA MKOA WA KILIMANJARO

Sunday, March 22, 2015
  • Afanya ziara wilaya ya Siha
  • Aipongeza wilaya hiyo kwa maendeleo ya kasi
  • Awapongeza Viongozi kwa kufikisha maji safi na salama kwenye kila kijiji
  • Ampongeza Mbunge wa Jimbo la Siha kwa juhudi zake za kuboresha Afya na Elimu
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akivishwa skafu wakati wa mapokezi wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na viongozi wa CCM wilaya ya Siha wakati wa mapokezi yaliyofanyika Makiwaru wilaya ya Siha.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Mbunge wa Jimbo la Siha Aggrey Mwanri (kushoto) na Mbunge wa Viti Maalum Betty Machangu (kulia) wakiondoka eneo la shule ya Nuru Sekondari baada ya kushiriki ujenzi wa bwalo la chakula pamoja na vyumba vya madarasa vya kidato cha tano na cha sita.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia bwawa la maji kwa ajili ya umagiliaji kijiji cha Kishisa  ambalo lina uwezo wa kubeba lita 5,520,000,likiwa na uwezo wa kumwagilia hekta 200 na linanufaisha kaya 696.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Kaimu Mganga Mfawidhi wa hospitali ya wilaya ya Siha Dk.Loveland Makundi
 Mbunge wa Jimbo la Siha na Naibu Waziri wa TAMISEMI Ndugu Aggrey Mwanri akimuelezea Katibu Mkuu wa CCM namna ambavyo jimbo lake linaboresha huduma za afya.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoka kukagua maabara ya kisasa ya hospitali ya wilaya ya Siha,kulia ni Mbunge wa Jimbo la Siha na Naibu Waziri wa TAMISEMI Ndugu Aggrey Mwanri

 Hospitali ya wilaya ya Siha.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa wilaya ya Siha kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa CCM wilaya ambapo alisisitiza CCM itaendelea kutetea haki za wanyonge.
 Wananchi wa wilaya ya Siha wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana huku wakinyeshewa na mvua mvua
 Meza kuu wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana licha ya mvua kuwanyeshea.
 Waandishi wakiendelea kuchukua matukio wakati wa mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na wananchi wa wilaya ya Siha wakiwa wamejikinga mvua na miamvuli.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kushoto) akifurahia jambo pamoja na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Siha Ndugu Oscar Jeremia Temi na MNEC wa wilaya ya Siha wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kwenye uwanja wa CCM wilaya ya Siha.
 Mbunge wa Jimbo la Siha na Naibu Waziri wa TAMISEMI Ndugu Aggrey Mwanri akihutubia wakazi wa wilaya ya Siha kwenye mkutano wa hadhara ambao mgeni wa heshima alikuwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Wananchi wakifuatilia mkutano
 Mbunge wa Viti Maalum Betty Machangu akihutubia wananchi na kuwaambia wajiandikishe kwenye daftari la kudumu la wapiga kura kwani ndio fursa pekee ya wao kupiga kura wakati Katiba na chaguzi zingine za Serikali.

 Wasanii wa Kimaasai wakiimba mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 Sehemu ya umati wa watu
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipanda mti mara baada ya kuifungua ofisi ya CCM wilaya ya Siha.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimia wananchi wakati wa ufunguzi wa ofisi ya CCM wilaya.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kama ishara ya kufungua ofisi ya CCM wilaya ya Siha.

Chapisha Maoni

0 Maoni