Unordered List


KINANA ;MOSHI ACHENI USHABIKI WA KISIASA


Tuesday, March 31, 2015
  • Wafanyabiashara wafunga barabara
  • Walalamikia kufungiwa soko la kati kwa mwaka mzima
  • Kwa miaka 20 upinzani hamna walilofanya Moshi mjini
  • Nape awaambia stukeni wananchi,chagueni viongozi watakaowaletea maendeleo
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia vijana wa boda boda ,Stendi Kuu kata ya Mawenzi ambapo aliwaambia kuwa boda boda ni sehemu ya kupata kipato hivyo inabidi wafanye shughuli yao hiyo kwa umakini mkubwa ,ikiwa kudumisha umoja, kufuata sheria, kujisajiri na kutambulika na mamlaka husika ,kuaminika ili waweze kukopesheka.
 Katibu wa Umoja wa Boda Boda Moshi mjini akisoma risala kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye mkutano uliofanyika ,Stendi Kuu kata ya Mawenzi Moshi mjini.
 Wafanyabiashara wa soko la kati,Moshi mjini wakiwa wamefunga njia kuzuia msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana usipite mpaka wawasilishe kero yao ya kufungiwa soko kwa mwaka mzima na uongozi wa halmashauri ya mji kwa maelezo ya kupisha ukarabati ambao haujafanyika.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisoma ujumbe ulioandikwa kwenye mabango na wafanyabiashara wa soko la kati,Moshi mjini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisoma risala ya wafanyabiashara wa soko la kati,Moshi mjini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wafanya biashara ambao soko lao limefungwa kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kuingia kwenye soko la kati, Moshi mjini mkoani Kilimanjaro ambalo lilifungwa kupisha ukarabati ambao mpaka sasa ni mwaka 1 hakuna kilichofanyika na wafanyabiashara wanaishi maisha magumu.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wafanyabiashara wa soko la kati ambalo limefungwa kwa mwaka mzima sasa.
 Ukuta wa soko la kati Moshi mjini ukiwa na matangazo yanayozuia kufanya biashara
 Katibu wa Vikoba kata ya Kongoroni Mariam Chawapoma akisoma risala ya kikundi chao kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana .
 Wanachama wa Vikoba wakishangilia jambo wakati wa mkutano na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wanachama wa Vikoba kata ya Makongoroni ambapo alishiriki kuzindua vikoba 11 vyenye wanachama 330,Kata ya Makongoroni,Moshi mjini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kufyatua matofali baada ya kutembelea kikundi Vijana cha Kata ya Miembeni
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na umati wa akina mama Lishe wa Njoro,Moshi mjini.


 Wajasiriamali na mama lishe wakishangilia ujio wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katika kata yao ya Njoro.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wajasiriamali pamoja na mama lishe.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye pamoja na Mwenyekiti wa CCM mkoa Ndugu Idd Juma
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikatiza kwenye maji wakati akielekea kwenye eneo la mkutano wa hadhara Bomambuzi viwanja vya shule ya msingi Mandela.
 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kutoka wilaya ya Moshi mjini Ndugu Aggrey Marealle akihutubia wananchi wa Moshi mjini ambapo aliwaambia kuwa wakati umefika wa kufanya mabadiliko ya kweli kwa kuchagua CCM kuongoza mji wa Moshi.


 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Moshi mjini mkutano wa hadhara Bomambuzi viwanja vya shule ya msingi Mandela na kuwaambie wastuke sasa wasiendelee kukandamizwa na viongozi wasiojali maendeleo yao.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa Moshi mjini kwenye mkutano wa hadhara Bomambuzi viwanja vya shule ya msingi Mandela na kuwaambia kuwa wamekuwa na ushabiki kwa miaka 20 imefika wakati sasa kuamua kuchagua maendeleo kwa manufaa ya maisha yao
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia picha ya gari alilotumia Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kabala halijafanyiwa ukarabati na Chuo cha Ufundi Veta, Moshi mjini.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijaribu kuendesha gari alilotumia Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wakati wa harakati za kutafuta uhuru,kulia ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiteremka kwenye gari alilotumia Baba wa Taifa wakati wa harakati za kutafuta uhuru.


Wananchi wakiuaga msfara wa  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mara baada ya mkutano kumalizika kwenye viwanja vya shule ya msingi Mandela,Bomambuzi, Moshi Mjini.

Chapisha Maoni

0 Maoni