Njia 3 muhimu katika ujenzi wa uchumi wa gesi Tanzania
Na Dk. A. Massawe
YA KWANZA
Mojawapo 
ya njia zitakazofanikisha matumizi ya gesi yetu asilia hapa chini yawe 
yenye tija zaidi ni ile ya kuisambaza maeneo yote nchini kwa kuanzia na 
miji mikuu ya kanda au mikoa kwa ajili ya matumizi ya majumbani na 
viwandani na kuzalisha umeme kwa ajili ya matumizi ya pale pale 
unapozalishwa.
Kusafirisha
 gesi asilia kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam itakakotumika kuzalishia 
umeme, majumbani na viwandani ni sahihi tu kama umeme wote 
utakaozalishwa utatumika ndani ya ukanda wa Dar es Salaam.
Yaani, ni
 sehemu kidogo tu ya gesi asilia inayowasili Dar es Salaam ingebaki hapo
 hapo kwa ajili ya kuzalisha umeme na matumizi ya majumbani na viwandani
 ndani ya ukanda wa Dar es Salaam na kitakachosalia kiendelee na safari 
yake hadi kanda nyingine za Tanzania kuzalisha umeme na kwa ajili ya 
matumizi mengine ya moja kwa moja majumbani na viwandani kuendana na 
mahitaji ya kila kanda.
Lengo ni 
kuondokana upotevu mkubwa wa umeme na gharama kubwa ya kuusafirisha 
umbali mkubwa kutoka kanda moja ya Tanzania hadi nyingine, pia 
ikizingatiwa kwamba, zaidi ya umeme, kila kanda hapa Tanzania pia 
inahitaji gesi asilia kwa ajili ya matumizi ya moja kwa moja majumbani 
na viwandani kama Dar es Salaam.
Hivyo ni 
kosa kuzalisha umeme wa megawati 3000 hapa Dar es Salaam kutokana na 
gesi asilia ya Mtwara kwa ajili ya matumizi ya ukanda wa Dar es Salaam 
na kanda nyingine zilizoko mbali na Dar es Salaam kwani njia sahihi ni 
kusambaza uzalishaji wa umeme utokanao na gesi asilia kote nchini kwa 
kusambaza gesi asilia kote nchini kwa njia ya mabomba na kufunga mitambo
 midogo midogo ya uzalishaji wa umeme wa gesi asilia kwenye kila kanda 
kuendana na mahitaji halisi ya kanda.
Hivyo, 
cha muhimu zaidi kwenye kufanikisha matumizi ya gesi asilia hapa nchini 
yawe yenye tija tosha ni kujenga miundo mbinu ya mabomba kwa ajili ya 
usambazaji gesi asilia kikanda kote nchini itakakozalisha umeme na 
kutumika moja kwa moja majumbani na viwandani kikanda kuendana na 
mahitaji halisi kikanda ili kukwepa upotevu mkubwa wa umeme na gharama 
kubwa za kuusafirisha umbali mkubwa kutoka kanda hadi kanda, huku 
ikizingatiwa kwamba, zaidi ya umeme, kanda zote pia zinahitaji gesi 
asilia kwa ajili ya matumizi ya moja kwa moja majumbani na viwandani 
kama Dar es Salaam.(P.T)
YA PILI
Njia ya 
pili itakayofanikisha matumizi yenye tija ya raslimali ya gesi asilia 
iliyogundulika hapa nchini ni kutumia hisa za Serikali kwenye raslimali 
hiyo iliyoko ardhini ikisubiria kuanza kuvunwa kama rehani kuchukulia 
mikopo kwa ajili ya ujenzi wa mitambo ya kuzalishia umeme wa maji huko 
Stigler's na wa makaa ya mawe huko Mchuchuma na kwingineko. Ni matumizi 
yanayowezesha kurudisha mikopo na kuleta faida hata kabla uchimbaji wa 
gesi asilia iliyotumiwa kama rehani haujaenda mbali sana, huku 
ikizingatiwa kwamba maelfu ya megwati za umeme wa maji ambazo 
hazijavunwa huko Stiglers na kwngineko hapa nchi huwa zikipotea kila saa
 miaka nenda rudi wakati gesi asilia na makaa ya mawe yanaweza kusubiri 
ardhini hadi uvunwaji wake kwa ajili ya uzalishaji wa umeme utakapoanza.
YA TATU
Njia ya 
tatu itakayofanikisha matumizi yenye tija tosha ya raslimali ya gesi 
asilia iliyogundulika hapa nchini ni kuwekeza mapato ya serikali 
yatokanayo na uvunwaji wa ralimali yake ya gesi asilia kwenye mfuko 
endelevu ''Sovereignity Fund''wa kutolea mikopo yenye riba nafuu kwa 
sekta za umma (kwa ajili ya kuwekeza kwenye ujenzi na uendelezaji wa 
miundo mbinu ya kitaifa na kwenye makampuni ya kimataifa yaliyo mihimili
 mikuu ya maendeleo ya uchumi wa dunia kisayansi na kiteknolojia 
(kuiwezesha Tanzania kuwa sehemu ya wahimili wakuu wa uchumi wa dunia 
kisayansi na kitknolojia na kuwa mmojawapo ya wanaonufaika sana), na kwa
 sekta binafsi (kuwezesha ukuwaji wa ujasiriamali hapa nchini).
Ni 
kuzingatia kwamba raslimali ya gesi asilia hapa nchini ni urithi usio 
endelevu wa vizazi vyote vya Tanzania, na njia ya kuhakikisha matumizi 
yake ni yenye manufaa makubwa zaidi kwa vizazi vyote vya Tanzania ni 
kutumia mapato ya serikali yatokanayo na uvunwaji wake kama kianzio 
endelevu cha mikopo yenye riba nafuu kwa sekta binafsi na za umma kote 
nchini.
Chanzo:wavuti.com

 
1 Maoni
The Oil Drum | Electricity price differences between countries
www.theoildrum.com/node/7215