Unordered List


MGOMBEA MWENZA WA URAIS KWA TIKETI YA CCM, MAMA SAMIA AITEKA MOSHI MJINI, MAELFU WAHUDHURIA MKUTANO WAKE WA KAMPENI


 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia Suluhu akihutubia maelfu ya wananchi kwenye mkutano wake wa kampeni aliofanya kwenye Viwanja vya CCM Majengo, jimbo la Moshi mjini mkoani Kilimanjaro.
 Wananachi wakimpongeza mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassani baada ya kuhutubia mkutano wa kampeni kwenye viwanja vya CCM Majengo jimbo la Moshi mjini Mkoani Kilimanjaro.
 Wananchi wakishangilia kwa furaha wakati mgombea mwenza kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassani, alipohutubia mkutano wa kampeni kwenye viwanja vya CCM Majengo, jimbo la Moshi Mjini mkoani Kilimanjaro.
 Mwananchi akishangilia kwa nguvu zake zote, mgombea mwenza kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassani, alipohutubia mkutano wa kampeni kwenye viwanja vya CCM Majengo, jimbo la Moshi Mjini mkoani Kilimanjaro.
 Sehemu ya umati wa wananchi waliohudhuria mkutano huo wa kampeni
 Wananchi wakijimwayamwaya Uwanjani wakati wa mkutano huo
 Wananchi wenye mkutano huo wakinyoosha mikono kuahidi kuwachagua wagombea wa CCM, katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu, tangu mgombea wa Urais, Dk John Magufuli, Wabunge na madiwani
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akishiriki kucheza ngoma, wakati kikundi cha kina mama kutoka Moshi Mjini kilipotumbuiza wakati wa mkutano huo
 Mgombea Mwenza wa urais kwa tiketi ya CM, Mama Samia Suluhu akiwafurahia wananchi waliokuwa wakiselebuka mbele yake kwa furaha wakati wa mkutano huo.
 Vijana wakitoa burudani wakati wa mkutano huo
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM akimshukuru Mzee, Omari Mwariko (65) , baada ya mzee huyo kumkabidhi zawadi ya picha za Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na Mzee Kawawa , wakati wa mkutano huo
 Mgombea mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia, akizitazama vema picha alizokabidhiwa na mchoraji huyo, Mzee, Mwariko
 Kamanda wa Umoja wa Vijana, Kinondoni Dar es Salaam, Angela Kairuki, akishauriana jambo na Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia, wakati wa mkutano huo wa kampeni
 Mgombea Ubunge jimbo la Moshi Mjini kwa tiketi ya CCM,  Devis Mosha akimwaga sera wakati wa mkutano huo
 Mama Samia, akimpongeza Devis Mosha kwa hotuba nzuri
 Mbunge wa kuteuliwa, mkoa wa Tanga, Ummy Mwalimu, akiwaombea kura wagombea wa CCM, Dk. John Magufuli kwa upande wa Urais na wabunge na madiwani, wakati wa mkutano huo.
 Aliyekuwa mgombea Ubunge jimbo la Nkenge, mkoani Kagera, Asupta Mshanga, akiwaasa wananchi kuacha kuhama vyama baada ya kukosa nafasi za uongozi wanazoomba, alipohutubia mkutano huo, akisema " Mbona mimi licha ya kuwa ni mwanamke, baada ya kukosa nafasi ya kugombea ubunge kutokana na kura kutotosha nimetulia ndani ya Chama changu? Lakini wanaume wazima tena wengine wazee, wamekosa nafasi eti wanahama!"
 Mbunge wa Afrika Mashariki Angela Kizigha akizungumza, kumkaribisha mgombea Mwenza, Mama Samia kuzungumza, wakati wa mkutano huo. Katikati ni Katibu Mkuu wa UWT Amina makilagi
 Mgombea mwenza kwa tiketi ya CCM, Mama Samia akiwanadi wagombea wa Ubunge, Davis Mosha (Moshi Mjini), Innocent Meleck (Vunjo) na Dk. Siril Chami (Moshi Vijijini) wakati wa mkutano huo.
Wadau wakifuatilia hali ya mambo wakati wa mkutano huo.
 
Na Sufyan Omar 

Chapisha Maoni

0 Maoni