Unordered List


MUUNGANO WA WASANII TANZANIA WAMUAGA RAISI KIKWETE, MAGUFULI AHUDHURIA

 Muungano wa wasanii wameandaa hafla maalum ya kumshukuru na kumuaga Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na kumpongeza na kumkaribisha Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa kuteuliwa kuwa Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi,iliyoofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City 
Ukumbi wa Mlimani city kabla ya kuanza kwa sherehe hizo za kumuaga Dkt. JK na kumpongeza ndugu John Pombe Magufuli
 Mgombea wa Urais kupitia CCM  Dk. John Pombe Magufuli akiwasili kwenye ukumbi wa Mlimani City tayari kuhudhuria  hafla maalum ya kumshukuru na kumuaga Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mkuu wa wilaya wa kinondoni ndugu Paul Makonda akimkaribisha Mgombea uraisi wa CCM John Pombe Magufuli katika viwanja vya Mlimani city katika sherehe za kumuaga Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Kikwete.
Mgombea uraisi wa CCM ndugu John Pombe Magufuli akisaini katika kitabu cha mahudhurio katika ukumbi huo mbele ya mkuu wa wilaya ya kinondoni ndugu Paul Makonda.
Mgombea uraisi wa CCM akisalimiana na mbunge wa Bumbuli na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Mhe. January Makamba 
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli akiwa kwenye picha ya pamoja na Dimond ,Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ,Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Paul Makonda na Mbunge wa Jimbo la Bumbuli na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Mhe. January Makamba 

na Adnan

Chapisha Maoni

0 Maoni