Unordered List


COMRADE ASENGA ABUBAKAR; NAMUUNGA MKONO RAIS MAGUFULI, VIJANA TUPIGE KAZI

Kaimu Katibu Idara ya Hamasa, Sera, Utafiti na Mawasiliano UVCCM TAIFA, Ndugu Abubakar D. Asenga akisonga Ugali kwa Ajili  ya Kula na Vijana Wakulima.


We Mchange na Heche kwani pool table mnachezaga wapi hadi msema hamna maeneo ya kwenda kulima kuunga mkono kauli ya Rais Magufuli ya kufanya kazi?

Njooni Morogoro Mashamba mengi sana.kama hautaki shamba unaweza ata kuwa kibarua wa kulima na kung'0lea Mpunga  kwa mraba unapata malipo yako.

Kila mtu afanye kazi.asiefanya na asile
Mwalimu Nyerere wakati wake alisema wazi "marufuku wanyonyaji(kupe) wakuja kukaa mjini kutegemea kulishwa na shemeji zao ama kula kwa mjomba."
Mwalimu alisema wazi "watu hawa tu ndio wanahaki ya kunyonya wengine na kuishi kwa kutegemea wengine kama kupe anavyoishi kutegemea damu ya ng'ombe.
1.Watoto wadogo
2.wazee sana
3.walemavu"

VIJANA WENGINE WOTE TUFANYE KAZI
nimechoma sana ndizi  na mahindi barabarani Ifakara.
-Nimeuza karanga na mayai ya kuchemsha tangu shule ya msingi darasa la sita
-Nimeuza sana vinguo vya baba alivyokuwa akivishona Ifakara(mtoto wa fundicherahani)
-Nimeziba sana pancha gereji Kwa Mudi Kindindindi Ifakara.

NAMUUNGA MKONO RAIS MAGUFULI KUWA KIJANA YEYOTE MAKINI HAWEZI KUKOSA KAZI YA KUFANYA,
MSOME ERIC SHIGONGO NK

TUFANYE KAZI.
#HAPAKAZITU

Chapisha Maoni

0 Maoni