Unordered List


COMRADE ASENGA ABUBAKAR; WANACUF MATUSI HAITASAIDIA KUZUIA RAIS ASIAPISHWE

Kaimu Katibu Idara ya Hamasa, Sera, Utafiti na Mawasiliano UVCCM TAIFA, Ndugu Abubakar D. Asenga akizungumza na Vijana wa Hamasa Zanzibar.
Tunaomba mpuuze kwa mara nyingine uzushi unaosambazwa juu ya Umoja wa Vijana CCM na Kaimu Katibu Mkuu wake Ndugu Shaka Hamdu kwenye mitandao ya kijamii.

Tupo  Zanzibar Pemba na Unguja tunaendelea na hamasa ya vijana kushiriki kwa wingi Uwanja wa AMANI kesho kuhakikisha Rais Mteule Dr. Ally Mohammed Shein anaapishwa kwa salama na amani.

Tunajua kwa siasa za huku Zanzibar matusi ni ya kawaida kutoka kwa wapinzani Ila yamewapa taabu baadhi ya watu wabara.

WanaCUF hii ya matusi kwa Ndugu Shaka Hamdu hayatawasaidia kuzuia Rais asiapishwe.

Najua Salam za Jana za matembezi makubwa yalioongozwa Kaimu Katibu Mkuu UVCCM kwa kushirikiana na Idara ya Hamasa, Sera, Utafiti na Mawasiliano UVCCM TAIFA Pemba na unguja bado zinawapa kiwewe. Hamkuamini kuwa mmechokwa na malaki ya watu.

Tutawajibu vizuri baada ya kumaliza agenda ya kesho uwanja wa AMANI. Sasa hatoki mtu kwenye agenda
Masalaaam
Abubakar D. Asenga
Kaimu Katibu Idara ya Hamasa, Sera, Utafiti na Mawasiliano UVCCM TAIFA
Niulize kwa 0715429738
HAPA KAZI TU

Chapisha Maoni

0 Maoni