Unordered List


KATIBU WA UVCCM NYAMAGANA AFANYA ZIARA KATA YA ISAMILO

Katibu wa Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Ndugu Odilia Abraham Batimayo akizungumza na Vijana wa Kata ya Isamilo Wilaya ya Nyamagana Mkoa wa Mwanza.

Katibu wa Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Ndugu Odilia Abraham Batimayo (katikati) na Katibu Hamasa wa Wilaya (Kulia) wakielekea katika kikao na Vijana wa Kata ya Isamilo Wilaya ya Nyamagana Mkoa wa Mwanza.

Katibu wa Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Ndugu Odilia Abraham Batimayo(wa pili kushoto) akiwa Meza Kuu wakati anatambulishwa na Katibu Hamasa wa Wilaya katika kikao na Vijana wa Kata ya Isamilo Wilaya ya Nyamagana Mkoa wa Mwanza.

Katibu wa Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Nyamagana Ndugu Odilia Abraham Batimayo, aendeleza ziara yake ya kuimalisha jumuiya katika Kata ya Isamilo.

Akiambatana na Katibu Hamasa wa Wilaya, katibu Odilia amezungumza na kuwa hamasisha vijana juu ya uhai wa jumuiya na kuwahimiza vijana kuwa wazalendo katika kukitumikia chama na kuwa na umoja na mshikamano, lakini pia katika ziara yake hiyo amebaini changamoto mbali mbali zinazo wakabili vijana na kuzitolea ufafanuzi namna gani ya kuzitatua, moja ya changamoto kubwa ikiwa ni swala la ajira kwa vijana aliwaomba na kuwa hamasisha kwa haraka zaidi vijana waweze kuunda vikundi vya ujasiriamali ili kuweza kujikwamua kiuchumi na Kuwaahidi atakua nao bega kwa bega ili vijana kuweza kujiondoa katika hali ya kuwa tegemezi na kutafta fursa za kujikomboa kiuchumi.
 #HapaKaziTu

Chapisha Maoni

0 Maoni