Wanachama wa UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Mtwara, waliojitokeza kuja kuchukua kadi zao za Bima.
Kwa niaba ya UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Mtwara, nikiwa kama Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa natoa shukrani kwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mh. Halima Dendegu kwa kutekeleza ahadi yake ya kutoa kadi za Bima ya Afya kwa vijana 600 ambao walishiriki Kambi ya Vijana Mkoa mwaka jana.
Leo hii vijana hao wanafuraha sana kupata Kadi za Bima ya Afya ambazo zimelipiwa Mwaka mzima. Mungu akubariki sana Mh. Halima Dendegu kwa kutimiza ahadi yako kwa vijana wako wa Chama Cha Mapinduzi. CCM oyeeeeeeeèeeee |
0 Maoni