Unordered List


BREAKING NEWZZZ;MABULA AMBWAGA WENJE KESI YA UBUNGE JIJINI MWAZA LEO

Mbunge wa jimbo la Nyamagama,jijini Mwanza pichani akifurahia mara baada ya kutangazwa mshindi wa jimbo hilo na Mahakama kuu ya jijini Mwanza dhidi ya aliyekuwa Mgombea Ubunge wa jimbo hilo kupitia chama cha CHADEMA,Mh.Ezekiel Wenje.

Kesi ya kupinga matokeo ya Ubunge wa Jimbo la Nyamagana iliyofunguliwa na aliyekuwa mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje (CHADEMA) dhidi ya Mbunge wa sasa wa Nyamagana Stanslaus Mabula (CCM) ilikuwa ikiendelea katika mahakama Kuu Mwanza ambapo Ezekiel Wenje alifungua kesi hiyo akipinga matokeo yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yakimpa ushindi Mbunge wa sasa, Stanslaus Mabula. 

Leo April 8 2016, maamuzi ya kesi hiyo yametangazwa rasmi ambapo Mbunge Stanslaus Mabula ameshinda kesi hiyo, baada ya kubainika upande wa madai hauna ushahidi unaokidhi, kuithibitishia mahakama.

Sikiliza Sauti ya Mbunge wa Nyamagana  Mh.Stanslaus Mabula akizungumza na Wanannchi mara baada ya Uamuzi wa Mahakama kutolewa leo,ambapo yeye ameibuka mshindi dhidi ya aliyekuwa Mgombea Ubunge wa jimbo hilo kupitia chama cha CHADEMA,Mh.Ezekiel Wenje.  


 Wananchi wakifurahia ushindi wa Mbunge wa CCM Mh. Stanslaus Mabula.

Chapisha Maoni

0 Maoni