Kaimu Katibu Mkuu wa UMOJA wa Vijana Chama Cha Mapinduzi UVCCM Taifa, Ndugu Shaka Hamdu Shaka akipandisha Bendera ya CCM kuashiria uzinduzi rasmi wa Tawi la UVCCM. |
Amesema taasisi zote duniani huongozwa kwa mujibu taratibu , kanuni za msingi , kuheshimu katiba ili kukuza haiba ya uaminifu, uadilifu na utendaji bora.
Shaka aliyasema hayo kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na watendaji wa UVCCM ngazi za wilaya na Mikoa ya iliyopo kanda ya ziwa kilichofanyika Mkoani Tabora na Mwanza.
Alisema katika kufuata misingi na njia sahihi za usimamizi bora wa kiutendaji na kikazi zaidi, utendaji wa pamoja na uwajibikaji ni katika mambo makuu yanayohitajika katika UVCCM ya sasa.
Aliwakumbusha Kuwa kila mtumishi katika eneo lake la kazi ajione ana wajibu wa kukisaidia chama Cha Mapinduzi kufikia malengo yake sambamba na utunzaji wa mali na rasilimali za jumuiya ikiwemo na utii wa kununi maadili.
"Vipele havijitokezi katika kiwiliwili cha binadamu kama damu haichafuka, nitatumbua vipele vidogo baadae nitakamua majipu makubwa na kusafisha majeraha bila hofu yoyote kwa lengo la kuimarisha na kujenga jumuiya yenye kuendana na wakati tuliona ili tuendelee kuaminiwa ma vijana walio wengi zaidi"alieleza Shaka
Alisema hadhi na staha ya UVCCM iko katika kiwango cha juu kwasababu tayari imetoa viongozi wengi ambao wameshika madaraka ya utawala wa nchi katika nafasi mbalimbali za uongozi wa Taifa na medani za utawala wa sasa hivyo ni vyema ari hiyo kuendelezwa na viongozi waliopo sasa.
Kaimu Katibu Mkuu aliwatahadharisha watendaji hao kuwa kila mwanajumuiya, mtumishi na mtendaji yeyote anayefikiri uvccm ni kichaka cha kuficha uovu , ubadhirifu na ufisadi atajidanganya na daima hatapata nafasi ya kujificha katika uongozi wa sasa.
"Kila mmoja ajipime, ajichuje na kujitathmini mwenyewe kabla ya hatua za kikanuni hazijachukuliwa dhidi ya mtumishi au mtendaji , kama ulipora , ulishiriki kuvunja kanuni, kufuja mali au kuuza vitega uchumi, hukuna atakayekuhurumia " alisisitiza
Aliwataka watendaji wa UVCCM toka ngazi za Taifa hadi matawi kutambua kuwa ni wote wana wajibu wa kutii na kufuata kanuni na katiba pamoja na kuelewa mipaka ya kila mmoja katika kiwango na ukomo wa utendaji wake.
"Kama mtendaji hujui taratibu au kanuni mbalimbali na miongozo yetu usijifanye mwerevu , hujui jambo hebu uliza ili uelekezwe, kuuliza si ujinga na ukiujifanya kujua wakati hujui unaweza kuvurunda mambo"alisema Shaka huku watendaji wakiwa kimya kumsikiliza kwa makini .
Alisema msimamo wa Uvccm ambao umerithiwa toka enzi za TANU na ASP youth league kabla ya kuzaliwa Uccm ni dhana ya kiongozi kuongoza kwa mfano, kukosoa na kuwa tayari kukosolewa pia awe mzalendo, mtii anayejiheshimu na kuheshimu mwenzake.
Hata hivyo Shaka wakati akihitimisha kufikia mwisho ziara yake ya kukutana na watendaji wa UVCCM ambayo ilianza kanda ya kati mashariki,, nyanda za juu, kusini na kuhitimisha akiwa kanda ya ziwa amekutana na kuzungumza na watendaji wa mikoa na wilaya za Mwanza , Geita, Mara na Kagera Shinyanga, Kigoma Katavi, Tabora Simiyu, Rukwa amekamilisha kukutana na watendaji 173 wa wilaya na 32 wa mikoa.
Kwa upande wao watendaji hao wamelezea kuridhishwa na hatua iyo iltakayowaongezea ari na bidii katika utendaji wao.
0 Maoni