Unordered List


WABUNGE WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI KUHAMASISHA JAMII JUU YA FURSA ZA KIBIASHARA ZINAZOPATIKANA AFRIKA MASHARIKI

WABUNGE wa Jumuiya la Afrika Mashariki kuanza kuhamasisha jamii ili kujua fursa za Kibiashara zilizopo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Ameyasema hayo leo Mbunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Makongoro Nyerere wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, amesema kuwa wataanza kuhamasisha jamii katika soko la Kariakoo na Soko la Samaki la Feri jijini Dar es Salaam pamoja na vyombo vya habari mbalimbali.

Makongo amesema kusudi la kuelimisha jamii ili wafanyabishara waweze kufanya biashara katika nchi za Afrika Mashari kama Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.

Mbunge wa Bunge la Afrika Mashari Makongoro Nyerere akizungumza na waandishi wa habari(Hawapo pichani) jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na wabunge wa bunge la Afrika Mashariki kuanza kuhamasisha jamii kuchangamkia fursa za kibiashara zilizopo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, Kutoka kulia kwenda kushoto ni Mbunge wa bunge la Afrika Mashariki, Shyrose Banji, Miriam Yahaya Usi, Ndarakilo Kessy na Dk.Twaha Tasilima wakiwa katika mkutano huo leo.


Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Abdullah Mwinyi (Katikati)akifafanua jambo katika mkutano wa waandishi wa habari na wabunge wa bunge la Afrika Mashariki leo jijini Dar es Salaam.
Mbune wa Bunge la Afrika Mashariki, Nderakilo Kessy (aliyesimama )akizungumza na waandhishi wa habari hawapo pichani kuhusiana na wabunge hao kuanza kuhamasisha jamii juu ya Fursa zilizopo katika jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Shyrose Banji akizungumza kuhusiana na Fursa zilizopo katika Jumuiya ya Afrika Mashari.

Amesema kuwa frusa zilizopo kwa waalimu wa Lugha ya Kiswahili wanaweza kwenda kufundisha Kiswahili kwenye Nchi za Afrika Mashariki ikiwa ni Kenya Uganda, Rwanda, Burundi na Afrika ya kati ipo mbioni kujiunga na Umoja huo.

Amesema Lugha ya Kiswahili kwa sasa imeanza kushika karibu nchi zote za Afrika Mashariki na hii ndio fursa Kubwa tuliyo nayo.

 



Chapisha Maoni

0 Maoni