Unordered List


KAIMU KATIBU MKUU UVCCM NDUGU SHAKA HAMDU ATIKISA MKOA WA TABORA

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa, Ndugu Shaka Hamdu Shaka akitafakari jambo kwa kina.

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Ndugu Shaka Hamdu Shaka, akiwahutubia wananchi waliojitokeza katika Mkutano wa Hadhara wa kufunga Mbio za Bendera Mkoa wa Tabora.

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Ndugu Shaka Hamdu Shaka, Ndugu Seif Gulamali Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Tabora na Mkuu wa Idara ya Utawala UVCCM Taifa Ndugu Omary Mwanangwalu wakisaini Kitabu.

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Ndugu Shaka Hamdu Shaka, Ndugu Seif Gulamali Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Tabora na Mkuu wa Idara ya Utawala UVCCM Taifa Ndugu Omary Mwanagwalu wakizindua Shina.

Vijana wa UVCCM Mkoa wa Tabora Wakikimbiza Bendera.

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa, Ndugu Shaka Hamdu Shaka akipokea Bendera.

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Ndugu Shaka Hamdu Shaka, Ndugu Seif Gulamali Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Tabora na Mkuu wa Idara ya Utawala UVCCM Taifa Ndugu Omary Mwanagwalu wakiwapokea Vijana waliokuwa wanakimbiza Bendera.

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Ndugu Shaka Hamdu Shaka, Ndugu Seif Gulamali Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Tabora na Mkuu wa Idara ya Utawala UVCCM Taifa Ndugu Omary Mwanagwalu, wakiwa ongoza Vijana kukimbiza Bendera.

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Ndugu Shaka Hamdu Shaka, Ndugu Seif Gulamali Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Tabora na Mkuu wa Idara ya Utawala UVCCM Taifa Ndugu Omary Mwanagwalu, wakiwa ongoza Vijana kukimbiza Bendera

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Ndugu Shaka Hamdu Shaka, Ndugu Seif Gulamali Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Tabora na Mkuu wa Idara ya Utawala UVCCM Taifa Ndugu Omary Mwanagwalu wakiwasili.

Vijana wa Mkoa wa Tabora wakiapa kuwa Wanachama waaminifu kwa UVCCM.



Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Shaka Hamdu Shaka (MNEC) amekuwa mgeni rasmi katika kilele cha mbio za bendera Mkoani Tabora zilizoandaliwa na UVCCM mkoa huo. Mbio hizo zilizozinduliwa kimkoa mnamo tarehe 23 Mei 2015 na Mwenyekiti wa UVCCM mkoa Mhe Seif Gulamali (Mb) Mbiohizo za bendera zilikuwa na malengo yafuatayo: a) Kuunga mkono juhudi za Rais wa awamu ya 5 Mhe John Pombe Magufuli. b) Kumuaga Mwenyekiti wa CCM Jakaya Mrisho Kikwete na kumkaribisha Rais John Pombe Magufuli ambae anatarajiwa kukabidhiwa chama miezi michache ijayo. c) Kuendesha harambee za kuchangia madawati katika shule za Msingi. d) Kuwahamsisha vijana katika kuimarisha chama cha Mapinduzi na jumuiya zake. e) Kuwashukuru wananchi kwa kuichagua CCM katika uchaguzi wa mwaka 2015. f) Kuhamasisha vijana kujiunga katika vikundi vya ujasiriamali ili kujikwamua na ukali wa maisha. Katika mbio hizo za bendera zilizodumu kwa siku 7 kimkoa zilitanguliwa na mbio za kila wilaya zilizoanza tarehe 18 /05/2016 katika wilaya zote 7 za mkoa wa Tabora. Sambamba na kukimbiza bendera ya CCM na Ya Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania kulitanguliwa na uzinduzi wa mashina Ya UVCCM, ushiriki wa shughuli za kijamii, uzinduzi wa mashina ya mabalozi wa CCM, kuzindua vikundi vya wajasiriamali vijana sambamba na kuchagia madawati yenye lengo la Kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano. Jumla ya mashina 236, mashina ya vijana wajasiriamali 46, mashina ya mabalozi 365 yamezinduliwa sambamba na mikutano ya hadhara katika kata 224 za mkoa wa Tabora. Katika kilele kilichofanyika leo katika viwanja Stand Parking Nzenga Kaimu Katibu Mkuu Shaka alifika ofisi ya wilaya Nzenga na kusaini vitabu kisha kushiriki ufunguzi wa mashina ya wajasiriamali ya vijana na baadae kuhudhuria kilele cha kupokea mbio hizo maarufu kwa jina la Mbio za bendera Zilizo ambatana sambamba na kupokea wakimbiza bendera, kukabidhi kadi kwa wanachama wapya 3,700 ambapo wanachama19 waliotoka katika vyama vya upizani, kukabidhi vyeti vya shukrani na kisha kuhutubia mamia ya vijana waliohudhuria kilele hicho, aidha Kaimu Katibu Mkuu Shaka H Shaka alichangia shilllingi million moja ikiwa ni Kuunga mkono hatua ya serikali ya awamu ya tano katika kuwapatia madawati wanafunzi wa shule za Msingi.

Chapisha Maoni

0 Maoni