Kaimu Katibu Idara ya Hamasa, Sera, Utafiti na Mawasiliano UVCCM TAIFA, Ndugu Abubakar D. Asenga akifurahia Jambo na Vijana. |
Ilikuwa ofisi ya kata na baraza la Ardhi
Vijana wanakesi na wametelekezwa kisa ushabiki wao bila kufikiri
Tumechangia ujenzi wa Tofali kuanza msingi wa ujenzi wa kituo cha polisi cha Wilaya ya Kilombero Mkoani Morogoro
Tunamshukuru sana OCD wa polisi Wilaya na Diwani wa Kibaoni kwa kupokea mchango huo
Ni fedheha kubwa kuwa na kituo cha polisi cha wilaya wakati wa mvua askari wanaenda likizo kutokana na Mafuriko
Haikubaliki
Pia tumechangia Madawati 20 Ifakara na pia Rafiki zetu wa GSM Foundation wametuhidi kuchangia Madawati zaidi hivi karibuni
Wakati kesi yetu ya rufaa ya matokeo ya uchaguzi jimbo la Kilombero itaendelea ukumbi wa Halmashauri June 7
Nawasihi wananchi wote kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo.
Kumbukeni hii ni serikali ya hapa kazi tu inayoongozwa na Rais Makini Dk John Magufuli.Usipofanya kazi halali hautakula.Siasa inakuja baada ya Kazi.
HAPA KAZI TU
Huu mchezo hautaki Hasira.
Wenu
Abubakar Damian Asenga
Mtoto wa Fundi Cherahani
Kaimu Mkuu wa Idara ya Uhamasishaji,Sera,utafiti na Mawasiliano.
UVCCM MAKAO MAKUU
Maoni Meseji 0627968722
0 Maoni