Unordered List


COMRADE ASENGA ABUBAKAR; HUU MCHEZO HAUTAKI HASIRA

Kaimu Katibu Idara ya Hamasa, Sera, Utafiti na Mawasiliano UVCCM TAIFA, Ndugu Abubakar D. Asenga akifurahia Jambo na Vijana.
 Jengo mnaloliona nyuma ya Picha hizi ndilo lile jengo lililochomwa moto na vijana Mashabiki  Wa Chadema siku za mwisho za uchaguzi mkuu 2015
Ilikuwa ofisi ya kata na baraza la Ardhi

Vijana wanakesi na wametelekezwa kisa ushabiki wao bila kufikiri

Tumechangia ujenzi wa Tofali kuanza msingi wa ujenzi wa kituo cha polisi  cha Wilaya ya Kilombero Mkoani Morogoro

Tunamshukuru sana OCD wa polisi Wilaya na Diwani wa Kibaoni kwa kupokea mchango huo

Ni fedheha kubwa kuwa na kituo cha polisi  cha wilaya wakati wa mvua askari wanaenda likizo kutokana na Mafuriko
Haikubaliki

Pia tumechangia Madawati 20 Ifakara na pia Rafiki zetu wa GSM Foundation wametuhidi kuchangia Madawati zaidi hivi karibuni

Wakati kesi yetu ya rufaa ya matokeo ya uchaguzi jimbo la Kilombero itaendelea ukumbi wa Halmashauri June 7
Nawasihi wananchi wote kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo.

Kumbukeni hii ni serikali ya hapa kazi tu inayoongozwa na Rais Makini Dk John Magufuli.Usipofanya kazi halali hautakula.Siasa inakuja baada ya Kazi.
HAPA KAZI TU

Huu mchezo hautaki Hasira.

Wenu
Abubakar Damian Asenga
Mtoto  wa Fundi Cherahani

Kaimu Mkuu wa Idara ya Uhamasishaji,Sera,utafiti na Mawasiliano.
UVCCM MAKAO MAKUU

Maoni Meseji 0627968722




Chapisha Maoni

0 Maoni