Unordered List


MAKAMU MWENYEKITI CCM TANZANIA BARA MZEE PHILIP MANGULA ATEMBELEA KAMBI LA WAZALENDO WASOMI


Makamu mwenyekiti wa ccm Tanzania Bara Mzee Philip Mangula akitembelea kambi ya Vijana 53 wazalendo Wasomi wetu kutoka vyuo vikuu vya nje na ndani ya nchi walioungana kwa pamoja kufyatua matofali 45,000 kwa ajili kujenga mabweni 5 pamoja na nyumba 5 za walimu katika shule ya sekondari Nasibugani wilayani Mkuranga, mkoani Pwani.
Mkuu wa wilaya ya Mkuranga Mh Filberto Sanga alichukua hatua ya kuandaa kambi hii ya wazalendo kusaidia adha waliyokuwa wakipata wanafunzi wa shule ya Nasibugani gani ikiwemo kukosa mahala pa malazi huku baadhi yao kidato cha tano na sita wakilala katika chumba cha maabara.
Ripoti iliyosomwa na Katibu Mkuu wa Wazalendo Bw Daniel Sarungi inaelezea maisha ndani ya kambi na shughuli walizofanya ikiwemo
 Kufyatua matofali, Kusomba Mchanga, Kujipikia chakula, Kufundisha wanafunzi wa kidato cha V na VI, Kutoa huduma ya afya kwa wanakambi na wanafunzi, Mijadala ya maendeo na utawala bora pamoja na Kuhamasisha wanafunzi kujiunga na vilabu vya kupinga rushwa.
Report hiyo ya wazalendo pia imeomba serikali kama ikiona inafaa wale wote wanaopenda kufanya kazi serikalini waanze kwa kujitolea miezi 6 au mwaka mmoja ndipo waajiriwe kufuatana na taaluma zao.
Kambi inaongozwa na mwenyekiti wa kambi Mwita Nyarukururu, Makamu Mwenyekiti ambae ni Helen Madole pamoja na Katibu Mkuu wa wazalendo Daniel Sarungi.
Mlezi wa kambi ya wazalendo ni kamati ya ulinzi na usalama wilaya ikiongozwa na Mh DC Filberto Sanga.
Makamu mwenyekiti ccm Tanzania Bara  mzee Philip Mangula katika picha ya pamoja na kambi la wazalendo wasomi
Kambi ya wazalendo ilianza tarehe 28/09/2016 na mpaka sasa zaidi ya matofali 38,235 yako tayari na yamebaki matofali 6,765 tu.
 Makamu mwenyekiti ccm Tanzania Bara  mzee Philip Mangula akichakarika na Wazalendo wasomi
 Makamu mwenyekiti ccm Tanzania Bara  mzee Philip Mangula akiendelea kufanya kazi  na Wazalendo wasomi
Makamu mwenyekiti ccm Tanzania Bara  mzee Philip Mangula akiongea na Wazalendo wasomi.

Chapisha Maoni

0 Maoni