Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mama Samia Suluh
Hassani akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 30 la Taasisi ya
Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR), lililoanza leo Oktoba 4
na kilelele chake kukoma Oktoba 6,2016 katika Ukumbi wa Mikutano wa
Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu,Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Dkt
Mwele Malecela akizungumza mapema leo,alipokuwa akimkaribisha Makamu wa
Rais Mama Samia Suluhu Hassan,wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 30
lililoanza leo Oktoba 4 na kilelele chake kukoma Oktoba 6,2016 katika
Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es
Salaam.Katika kongamano hilo kauli mbiu yake ni “Uwekezaji katika tafiti
zenye ubunifu ili kufikia malengo endelevu ya dunia.”.
Dkt Mwele alieleza pia Mada zitakazojadiliwa ndani ya kongamano hilo
kuwa zitajikita zaid kwenye maeneo kama vile 1. Mkakati wa kuboresha
afya ya uzazi, ya mama, watoto wachanga na vijana. 2. Magonjwa sugu
yasiyoambukiza na changamoto zake,3. Kuendeleza mafanikio yaliyopatikana
katika mapambano dhidi ya UKIMWI, kifua kikuu na malaria,4. Usalama wa
Maji, Usafi wa mazingira na usafi binafsi,5. Mkakati wa afya moja katika
kudhibiti magonjwa ya milipuko,pamoja na 6. Magonjwa ya kitropiki
yasiyopewa kipaumbele.
Baadhi ya Washiriki wa kongamano hilo kutoka sehemu mbali mbali ndani
na nje ya chi wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo,ambapo mada
zaidi ya 200 zitawasilishwa na kujadiliwa kwa siku tatu.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mama Samia Suluh Hassani
akisalimiana na Naibu Waziri wa Afya,Dkt.Hamis Kigwangala,alipokuwa
akiwasili katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere,
jijini Dar es Salaam leo,kwa ajili ya uzinduzi wa Kongamano la 30 la
Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR),pichani
kushoto ni Mkurugenzi Mkuu,Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya
Binadamu Dkt Mwele Malecela
Baadhi
ya Washiriki wa kongamano hilo kutoka sehemu mbali mbali ndani na nje
ya chi wakiimba wimbo wa Taifa kabla ufunguzi wa Kongamano
hilo,lililoanza leo jijini Dar.
BOFYA HAPA KUSOMA HOTUBA YA MAKAMU WA RAIS KUHUSU KONGOMANO HILO BOFYA HAPA KUSOMA HOTUBA YA MKURUGENZI MKUU WA NIMR DKT MWELE MALECELE BOFYA HAPA
0 Maoni