Mfalme wa Morocco Mtukufu Mohammed VI leo tarehe 27 Oktoba, 2016 ameondoka Jijini Dar es Salaam na kuelekea Zanzibar.
Katika
Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam Mtukufu Mohammed
VI ameagwa na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt. John Pombe Magufuli aliyeambatana na Makamu wa Rais Mhe. Samia
Suluhu Hassan.
Akiwa
Jijini Dar es Salaam Mtukufu Mohammed VI aliyewasili nchini tarehe 23,
Oktoba 2016 kwa ziara ya kiserikali ya siku tatu amekutana na kufanya
mazungumzo na mwenyeji wake Rais Magufuli na pia viongozi hao
wameshuhudia utiaji saini wa mikataba 21 inayohusu ushirikiano wa
Tanzania na Morocco katika masuala mbalimbali ya kiuchumi.
Baada ya kumaliza ziara ya kiserikali ya siku tatu, Mtukufu Mohammed VI anaendelea na ziara binafsi hapa nchini.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
27 Oktoba, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akajadiliana jambo na Mfalme wa Morocco Mohamed VI kabla ya kuagana nae katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpokea Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakati alipowasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mfalme wa Morocco Mohamed VI kabla ya kuagana nae katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mfalme wa Morocco Mohamed VI kabla ya kuagana nae katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Mfalme wa Morocco Mohamed VI mara baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakiangalia bendi ya matarumbeta iliyokuwa ikitumbuiza katika ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono kuagana na mgeni wake Mfalme wa Morocco Mohamed VI aliyemaliza ziara yake ya kikazi na kuondoka jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakati nyimbo za Taifa zikiwa zinapigwa katika ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU
0 Maoni